Thursday, April 10, 2025

    COASTAL UNION YAICHARAZA SINGIDA BLACK STARS 2-1 MKWAKWANI


    WENYEJI, Coastal Union wameibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Singida Black Stars katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga.
    Mabao ya Coastal Union yamefungwa na viungo Josaphat Arthur Bada raia wa Ivory Coast aliyejifunga dakika ya 47 na Bakari Suleiman Msimu dakika ya 82, wakati bao pekee la Singida Bock Stars limefungwa na mshambuliaji Mghana, Jonathan Sowah kwa penalti dakika ya 76.
    Kwa ushindi huo, Coastal Union inafikisha pointi 28 na kupanda kwa nafasi ya tatu hadi ya 10, wakati Singida Black Stars inabaki na pointi zake 50 nafasi ya nne baada ya timu zote kucheza mechi 26.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: COASTAL UNION YAICHARAZA SINGIDA BLACK STARS 2-1 MKWAKWANI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry