// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); YANGA PRINCESS YAICHAPA SIMBA QUEENS 1-0 MWENGE - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE YANGA PRINCESS YAICHAPA SIMBA QUEENS 1-0 MWENGE - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
    Tuesday, March 18, 2025

    YANGA PRINCESS YAICHAPA SIMBA QUEENS 1-0 MWENGE


    TIMU ya Yanga Princess imeibuka na ushindi wa bao 1-0 na watani wao, Simba Queens katika mchezo wa Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge, Dar es Salaam.
    Pongezi kwa mfungaji wa bao hilo pekee, mshambuliaji wa Kimataifa wa Rwanda, Jeannine Mukandayisenga dakika ya 49 akimchambua kipa wa Kimataifa wa Kenya,  Winfrida Seda Ouko.
    Kwa ushindi huo, Yanga Princess inafikisha pointi 27, ingawa inabaki nafasi ya tatu ikizidiwa pointi saba na vinara, Simba Queens ambao pia ni mabingwa watetezi baada ya wote kucheza mechi 12.
    JKT Queens ipo katikati yao, Simba Queens na Yanga Princess ikiwa na pointi 32 katika nafasi ya tatu baada ya kucheza mechi 12 — na kesho inacheza na Mashujaa Queens Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, Mbweni, Dar es Salaam. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: YANGA PRINCESS YAICHAPA SIMBA QUEENS 1-0 MWENGE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry