KLABU ya Simba itamenyana na Al Masry ya Misri katika Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika mechi ya kwanza ikichezwa Aprili 3 Jijini Cairo na marudiano Aprili Aprili 10 Jijini Dar es Salaam.
Ikifanikiwa kuvuka hapo na kwenda Nusu Fainali itakutana na mshindi kati ya Stellenbosch ya Afrika Kusini na mabingwa, watetezi, Zamalek ya Misri.
Katika Ligi ya Mabingwa Afrika, mabingwa watetezi, Al Ahly watamenyana na Al Hilal ya Sudan, wakati MC Alger ya Algeria itamenyana na Orlando Pirates ya Afrika Kusini.
0 comments:
Post a Comment