// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); SINGIDA BLACK STARS YAENDELEZA UBABE, YAICHAPA KMC 2-1 LITI - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE SINGIDA BLACK STARS YAENDELEZA UBABE, YAICHAPA KMC 2-1 LITI - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Thursday, September 12, 2024

    SINGIDA BLACK STARS YAENDELEZA UBABE, YAICHAPA KMC 2-1 LITI


    WENYEJI, Singida Black Stars wameendeleza wimbo la ushindi katika Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara baada ya jioni ya leo kuichapa KMC mabao 2-1 Uwanja wa CCM Liti mjini Singida.
    Mabao ya Singida Black Stars inayofundishwa na Kocha Mbelgiji, Patrick Aussems yamefungwa na Josephat Bada dakika ya 40 na Elvis Rupia dakika ya 57, wakati la KMC limefungwa na Redemtus Mussa dakika ya 49.
    Huo unakuwa ushindi wa tatu kwa Singida Black Star baada ya awali kushinda mechi mbili ugenini dhidi ya Ken Gold 3-1 Jijini Mbeya na Kagera Sugar 1-0 mjini Bukoba.
    Kwa KMC huo unakuwa mchezo wa pili kucheza bila ushindi, kufuatia kulazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Coastal Union, nyumbani, Dar es Salaam wiki iliyopita. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SINGIDA BLACK STARS YAENDELEZA UBABE, YAICHAPA KMC 2-1 LITI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top