// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); MWANAMICHEZO MWINGINE WA TANZANIA ATOLEWA OLIMPIKI - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE MWANAMICHEZO MWINGINE WA TANZANIA ATOLEWA OLIMPIKI - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Monday, August 05, 2024

    MWANAMICHEZO MWINGINE WA TANZANIA ATOLEWA OLIMPIKI



    MWANAMICHEZO wa tatu wa Tanzania, Sophia Anisa Latiff Jumamosi alitupwa nje kwenye Michezo ya Olimpiki kufuatia kumaliza wa mwisho katika waogeleaji nane mita 50 (Freestyle) kwa wanawake akitumia muda wa sekunde 28:42 na kuweka rekodi mpya binafsi.
    Mshindi, Jovana Kuljaca wa Montenegro alitumia sekunde 27:19 na wa pili Christina Rach wa Dubai akitumia sekunde 27:20, huku Kennice Aphenie Greene wa St Vincent & the Grenadines akimalza wa tatu kwa kutumia sekunde 27:23.  
    Sophia anamfuatia muogeleaji mwenzake wa Tanzania, Collins Phillip Saliboko aliyetolewa katika mita 100 (Freestyle) kwa wanaume Julai 30 baada ya kumaliza katika nafasi ya saba akitumia sekunde 53:38, wakati mshindi wa kwanza Ovesh Purahoo wa  Mauritius alitumia sekunde 52:22, ikiwa ni tofauti ya sekunde 1:16 tu.
    Sasa matumaini ya Watanzania kwenye Michezo hiyo inayoendelea Jijini Paris yamebaki kwa wanariadha wanne wa mbio ndefu pekee, Alphonce Felix Simbu na Gabriel Geay, wanaume na Jackline Juma Sakilu na Magdalena Crispin Shauri wanawake.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MWANAMICHEZO MWINGINE WA TANZANIA ATOLEWA OLIMPIKI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top