• HABARI MPYA

    Wednesday, July 03, 2024

    SIMBA SC YASAJILI KIUNGO MUIVORY COAST ‘DOGO’ WA MIAKA 22 TU


    KLABU ya Simba imeendelea kujiimarisha kuelekea msimu ujao baada ya kumtambulisha kiungo mshambuliaji Muivory Coast, Jean Charles Ahoua (22) kutoka Stella Club d'Adjamé ya kwao, Abidjan.
    Huyo anakuwa mchezaji wa nne mpya baada ya beki mzawa, Lameck Elias Lawi (18) kutoka Coastal Union, winga Mzambia, Joshua Mutale (22) kutoka Power Dynamos ya Zambia na mshambuliaji Mganda, Steven Mukwala (24) kutoka Asante Kotoko ya Ghana.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA SC YASAJILI KIUNGO MUIVORY COAST ‘DOGO’ WA MIAKA 22 TU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top