KLABU ya Simba imeendelea kujiimarisha kuelekea msimu ujao baada ya kumtambulisha kiungo mshambuliaji Muivory Coast, Jean Charles Ahoua (22) kutoka Stella Club d'Adjamé ya kwao, Abidjan.
Huyo anakuwa mchezaji wa nne mpya baada ya beki mzawa, Lameck Elias Lawi (18) kutoka Coastal Union, winga Mzambia, Joshua Mutale (22) kutoka Power Dynamos ya Zambia na mshambuliaji Mganda, Steven Mukwala (24) kutoka Asante Kotoko ya Ghana.
0 comments:
Post a Comment