// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); SIMBA NA YANGA AGOSTI 8 MKAPA NGAO YA JAMII, AZAM NA COASTAL NI ZANZIBAR - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE SIMBA NA YANGA AGOSTI 8 MKAPA NGAO YA JAMII, AZAM NA COASTAL NI ZANZIBAR - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Thursday, July 18, 2024

    SIMBA NA YANGA AGOSTI 8 MKAPA NGAO YA JAMII, AZAM NA COASTAL NI ZANZIBAR

    MECHI za Nusu Fainali ya Ngao ya Jamii zitachezwa Agosti 8, Azam FC dhidi ya Coastal Union kuanzia Saa 10:00 jioni Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar na Simba dhidi ya Yanga kuanzia Saa 1:00 usiku Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
    Mechi zote za mwisho zitachezwa Agosti 11, ikitangulia ya kusaka mshindi wa tatu Saa 9:00 Alasiri na kufuatiwa na Fainali Saa 1:00 Usiku.
    Mfumo wa timu nne katika Ngao ya Jamii ulianza rasmi msimu uliopita kwa bingwa wa Ligi Kuu kucheza na mshindi wa tatu, na mshinfi wa pili kumenyana na mshindi wa nne.
    Simba SC ndio waliokuwa mabingwa msimu uliopita wakiifunga kwa penalti 3-1 dhidi ya watani, Yanga kufuatia sare ya bila kufungana ndani ya dakika 90, wakati Azam FC ilimaliza nafasi ya tatu baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Singida Fountain Gatew Uanja wa Mkwakwani Jijini Tanga.
    Simba ilifika Fainali kwa ushindi wa penalti pia 4-2 dhidi ya Singida Fountain Gate huku Yanga wakiifunga Azam FC 2-0.




    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA NA YANGA AGOSTI 8 MKAPA NGAO YA JAMII, AZAM NA COASTAL NI ZANZIBAR Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top