// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); NI HISPANIA BINGWA EURO 2024, YAICHAPA ENGLAND 2-1 UJERUMANI - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE NI HISPANIA BINGWA EURO 2024, YAICHAPA ENGLAND 2-1 UJERUMANI - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Monday, July 15, 2024

    NI HISPANIA BINGWA EURO 2024, YAICHAPA ENGLAND 2-1 UJERUMANI


    HISPANIA imefanikiwa kutwaa Kombe la Mataifa ya Ulaya, Euro 2024 baada ya ushindi wa 2-1 dhidi ya England  usiku wa Jumapili Uwanja wa Olympia Jijini Berlin nchini Ujerumani.
    Nyota mwenye asili ya Ghana, Nicholas ‘Nico’ Williams Arthuer (22) alianza kuwafungia La Roja dakika ya 47 akimalizia pası nzuri ya winga mwenzake mwenye asili ya Afrika,  Lamine Yamal Nasraoui Ebana (17) ambaye baba yake anatokea Morocco na mama yake, Sheila Ebana anatokea Equatorial Guinea.
    Lakini Cole Jermaine Palmer (22) akaisawazishia Three Lions dakika ya 72 akimalizia pasi ya kiungo mwenzake mshambuliaji, Jude Victor William Bellingham baada ya kazi nzuri ya Bukayo Ayoyinka Temidayo Saka mwenye asili  Nigeria, Bukayo Ayoyinka Temidayo Saka.
    Shujaa wa Hspania alikuwa ni winga pia, Mikel Oyarzabal Ugarte aliyefunga bao la ushindi dakika ya 86 baada ya kazi nziri ya beki wa Chelsea, Marc Cucurella Saseta.
    Hilo linakuwa taji la nne kwa Hispania baada ya awali kulitwaa katika miaka ya 1964, 2008 na 2012, wakati kwa England hii ni mara ya pili wanafungwa katika Fainali kufuatia 2020 walipokuwa wenyeji kuchapwa kwa penalti 3-2 baada ya sare ya 1-1 na Italia Uwanja wa Wembley Jijini London.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NI HISPANIA BINGWA EURO 2024, YAICHAPA ENGLAND 2-1 UJERUMANI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top