• HABARI MPYA

    Monday, June 24, 2024

    SIMBA SC YATANGAZA RASMI KUACHANA NA HENOCK INONGA BAKA ‘VARANE’


    KLABU ya Simba imeachana na beki wa Kimataifa was Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Henock Inonga Baka ‘Varane’ baada ya kuwatumikia Wekundu wa Msimbazi tangu mwaka 2021 alipowasili kutoka DC Motema Pembe ya kwao, Kinshasa. 
    Huyo anakuwa mchezaji wa sita kutemwa Simba baada ya beki mwingine wa katı, Kennedy Wilson Juma, viungo, Mrundi Saido Ntibanzokiza, Luis Jose Miquissone wa Msumbiji na washambuliaji John Raphael Bocco na Shaaban Iddi Chilunda.
    Tayari Simba SC imemtambulisha mchezaji mmoja tu mpya, beki chipukizi wa katı, Lameck Elias Lawi (18) kutoka Coastal Union ya Tanga.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA SC YATANGAZA RASMI KUACHANA NA HENOCK INONGA BAKA ‘VARANE’ Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top