• HABARI MPYA

    Thursday, June 27, 2024

    SHIME AITA 20 TWIGA STARS YA KUCHEZA NA TUNISIA YANGA PRINCESS HAKUNA HATA MMOJA


    KOCHA Bakari Nyundo Shime ameita wachezaji 20 kuunda kikosi cha timu ya Taifa ya wanawake, Twiga Stars kwa ajili ya michezo miwili ya kirafiki dhidi ya Tunisia na Botswana mapema mwezi ujao.
    Katika kikosi hicho kitakachoingia kambini Julai 1 hakuna hata mchezaji mmoja wa Yanga Princess, huku mabingwa Simba Queens wakiwa na wachezaji wawili pekee.
    JKT Queens imeendelea kuwa klabu yenye wachezaji wengi zaidi Twiga Stars, saba huku wengine wakitoka Alliance Girls, Bunda Queens na Amani Queens mmoja kila timu, wakati wengine ni wanaocheza klabu mbalimbali nje ya Tanzania.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SHIME AITA 20 TWIGA STARS YA KUCHEZA NA TUNISIA YANGA PRINCESS HAKUNA HATA MMOJA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top