• HABARI MPYA

    Wednesday, June 19, 2024

    MANGUNGU ATEUA ‘MJUMBE MZITO’ KUINGIA KWENYE BODI SIMBA SC


    Dk. Kailima Ramadhani Kombwey (kulia) ni mtumishi wa muda wa mrefu wa Serikali tangu awamu ya nne chini ya Rais Dk. Jakarta Mrisho Kikwete (kushoto).

    MWENYEKITI wa klabu ya Simba, Murtaza Mangungu amemteua Dk. Kailima Ramadhani Kombwey kuwa Mjumbe wa Bodi ambaye ataungana na Wajumbe wateule upande wa Mwekezaji, Mohamed ‘Mo’ Dewji.
    Dk. Kailima Ramadhani Kombwey kwa sasa ni Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) ambaye aliteuliwa Februari mwaka jana na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan akichukua nafasi ya Dk. Wilson Mahera Charles aliyehamishiwa kwenye nafasi ya Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, TAMISEMI.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MANGUNGU ATEUA ‘MJUMBE MZITO’ KUINGIA KWENYE BODI SIMBA SC Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top