BAO pekee la winga Mjamaica, Leon Bailey dakika ya 74 limetosha kuipa Aston Villa ushindi wa 1-0 dhidi ya mabingwa watetezi, Manchester City katika mchezo wa Ligi Kuu ya England usiku wa kuamkia leo Villa Park Jijini Birmingham.
Kwa ushindi huo kwenye mchezo baina ya makocha wa Hispania, kikosi cha Kocha Unai Emery kinafikisha pointi 32 na kupanda nafasi ya tatu, kikiishushia timu ya Pep Guardiola nafasi ya nne Man City wa kubaki na pointi zao 30 baada ya wote kucheza mechi 15.
0 comments:
Post a Comment