Ilianza Coastal Union kuitupa nje Simba SC kwa kuilaza 1-0, bao pekee la Mgaya Khamis dakika ya 48.
Ikifuatia Mbeya Kwanza kuitoa Yanga kwa kuichapa 1-0 pia, bao pekee la Ahmed Hassan dakika ya 51.
Mechi nyingine za Robo Fainali, wenyeji, Azam FC walikwenda Nusu Fainali kwa ushindi wa penalti 6-5 baada ya sare ya 1-1.
Katika mchezo wa kwanza, mabingwa watetezi, Mtibwa Sugar waliitupa nje Geita Gold kwa penalti 4-2 baada ya sare ya 1-1.
Nusu Fainali ni Ijumaa, Mbeya Kwanza na Coastal Union na Azam FC dhidi ya Mtibwa Sugar hapo hapo Azam Complex.
0 comments:
Post a Comment