TIMU ya Azam FC imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi ya Vijana chini ya umri wa miaka 17 baada ya ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya Pan African kwenye mchezo wa mwisho leo Jijini Dar es Salaam.
Azam Academy imemaliza na pointi 34 baada ya kushinda mechi 11 na kutoa droo moja, mbele ya Simba waliomaliza nafasi ya pili kwa pointi zao 21 sawa na JMK Park wa tatu, wakati Yanga iliyomaliza na pointi 19 ni ya nne.
0 comments:
Post a Comment