BAO la penalti la Deo Minga dakika ya 75 limetosha kuipa Mbeya Kwanza ushindi wa 1-0 dhidi ya Tanzania Prisons leo Uwanja wa Maji Maji mjini Songea mkoani Ruvuma.
Mbeya Kwanza inafikisha pointi 21 katika mchezo wa 22 nafasi ya 15 kwenye ligi ya timu 16, ikiizidi wastani wa mabao tu Coastal Union inayoshika mkia, ingawa ina mechi moja mkononi.
Tanzania Prisons inabaki na pointi zake 22 za mechi 22 sasa nafasi ya 14.
Ikumbukwe timu mbili zitateremka daraja mwishoni mwa msimu na mbili zitakwenda kucheza na timu za Championship kuwania kubaki Ligi Kuu.
0 comments:
Post a Comment