// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); BURIANI KAPTENI ZACHARIA HANS POPPE - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE BURIANI KAPTENI ZACHARIA HANS POPPE - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Monday, September 13, 2021

    BURIANI KAPTENI ZACHARIA HANS POPPE

    MWILI wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya klabu ya Simba, Zacharia Hans Poppe aliyefariki dunia Ijumaa jioni hospitali ya Aga Khan Jijini Dar es Salam umeagwa leo katika ukumbi wa Karimjee, Dar es Salaam.
    Viongozi mbalimbali wa michezo wakiongozwa na Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Leodegar Chilla Tenga wameshiriki zoezi hilo pamoja na wanachama wa Simba SC.
    Mwili huo unatarajiwa kusafirishwa kesho kwa mazishi yatakayofanyika Jumatano Kihesa, Mkimbizi mkoani Iringa.
    Hans Poppe alizaliwa Oktoba 15, mwaka 1956 mjini Dar es Salaam na kukulia mkoani Iringa na baada ya kumaliza elimu ya sekondari, alijiunga na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) ambako alifikia cheo cha Kapteni, kabla ya kuachishwa kazi na kuhukumiwa kifungo cha maisha jela, kwa tuhuma za uhaini, dhidi ya serikali ya awamu ya kwanza, ya hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, mwaka 1983.




    Lakini mwaka 1995, Zacharia aliachiwa huru kwa msamaha wa rais wa awamu ya pili, Alhaj Ally Hassan Mwinyi, mwezi mmoja kabla hajamuachia Ikulu ya Tanzania, Benjamin William Mkapa, rais wa awamu ya tatu na baada ya hapo akajiajiri kwa kuanzisha kampuni ya usafirishaji ZH Poppe ambayo imekuwa kubwa barani.
    Amekuwa mpenzi wa Simba SC tangu miaka ya 1970, akiwa kijana mdogo na zaidi mwenyewe aliwahi kusema, mechi ambayo ilimfanya ajitamke rasmi yeye ni Simba damu ilikuwa dhidi ya wapinzani wa jadi, Yanga Juni 23, mwaka 1973, ambayo Wekundu wa Msimbazi, walishinda 1-0, bao pekee la Haidari Abeid ‘Muchacho’ dakika ya 68.
    Amekuwa Mjumbe Mteule wa Kamati ya Utendaji tangu mwaka 2010 na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili tangu 2012 kabla ya kuwa Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi katika mfumo mpya wa uendeshwaji klabu tangu mwaka jana. RIP Hans Poppe.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BURIANI KAPTENI ZACHARIA HANS POPPE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top