MCHEZAJI Bora Chipukizi wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, Novatus Dismas atajiunga na klabu ya Maccabi Tel-Aviv ya Israel baada ya kufuzu majaribio.
Novatus anakuwa mchezaji wa pili kuuzwa na Azam FC msimu hu, baada ya wiki chache zilizopita kumpiga bei mshambuliaji Shaaban Iddi Chilunda, aliyejiunga na Mouloudia d'Oujda ya Morocco.
Dismass amekuzwa kwenye kituo cha kukuza vipaji cha Azam FC sambamba na Chilunda kabla ya wote kupandishwa timu kubwa kwa wakati tofauti.
Azam FC imesema itaendelea kuthamini na kuendeleza vipaji vya wachezaji waliokuwa kwenye kikosi cheke na haitasita kufanikisha ndoto zao za kwenda kucheza nje ya nchi pale mchezaji anapopata timu na taratibu zote zinapofuatwa na timu husika.
0 comments:
Post a Comment