• HABARI MPYA

        Saturday, August 24, 2019

        KAGERA SUGAR, NAMUNGO, POLISI ZAANZA VYEMA LIGI KUU, MBEYA CITY NA PRISONS 0-0

        MATOKEO TOTE MECHI ZA LIGI KUU LEO
        Kagera Sugar 2-0 Biashara United
        Polisi Tanzania 1-0 Coastal Union
        Mbeya City 0-0 Tanzania Prisons
        Mbao FC 1-1 Alliance FC
        Namungo 2-1 Ndanda FC
        MECHI ZA KESHO
        Mwadui FC V Singida United Saa 10:00 Jioni
        Lipuli FC V Mtibwa Sugar Saa 10:00 Jioni

        Na Mwandishi Wetu, MUSOMA
        TIMU ya Kagera Sugar ya Bukoba imeanza vyema Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya ushindi wa 2-0 dhidi ya wenyeji, Biashara United Uwanja wa Karume mjini Musoma mkoani Mara jioni ya leo. 
        Mabao ya Kagera Sugar inayofundishwa na beki wa zamani wa kimataifa wa Tanzania leo yamefungwa na Yussuf Mhilu dakika ya 14 na Awesu Awesu dakika ya 90 na ushei katika mchezo ambao wenyeji walikosa penalti iliyopigwa na Jarome Lambere.
        Mechi za Ligi Kuu leo, bao pekee la Mohamed Mkopi dakika ya 33 liliwapa ushindi wa 1-0 Polisi Tanzania dhidi ya Coastal Union Uwanja wa Ushirika mjini Moshi mkoani Kilimanjaro, wakati Mbeya City imetoa sare ya 0-0 na mahasimu wao wa Jiji, Tanzania Prisons Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.
        Nayo Mbao FC ililazimishwa sare ya 1-1 na wapinzani wao wa Jiji, Alliance FC Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza. Mbao FC walitangulia kwa bao la Paschal Frank dakika ya 28, kabla ya Ibrahim Said kujifunga dakika ya 90 na ushei kuipa Alliance bao la kusawazisha.
        Nayo Namungo FC ikaanza vyema kwa ushindi wa 2-1 dhidi ya Ndanda FC Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mabao yake yote yakifungwa na Lucas Kikoti huku la wageni likifungwa na Omar Ramadhan. Ndanda walimaliza pungufu baada ya Hemed Koja kutolewa kwa kadi nyekundu.
        Ligi kuu itaendelea kesho kwa mechi mbili, Mwadui FC wakiwakaribisha Singida United mkoani Shinyanga na Lipuli FC wakiwa wenyeji wa Mtibwa Sugar Uwanja wa Samora, Iringa.
        • Blogger Comments
        • Facebook Comments

        0 comments:

        Item Reviewed: KAGERA SUGAR, NAMUNGO, POLISI ZAANZA VYEMA LIGI KUU, MBEYA CITY NA PRISONS 0-0 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry