// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); MAN UNITED YAPEWA PSG 16 BORA LIGI YA MABINGWA ULAYA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE MAN UNITED YAPEWA PSG 16 BORA LIGI YA MABINGWA ULAYA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

        Monday, December 17, 2018

        MAN UNITED YAPEWA PSG 16 BORA LIGI YA MABINGWA ULAYA

        TIMU ya Manchester United itamenyana na Paris Saint-Germain katika hatua ya 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
        Timu nyingine tatu za England nazo zimepangiwa wapinzani wagumu kutoka Ujerumani katika hatua hiyo.
        Liverpool imepangiwa Bayern Munich, wakati Manchester City itamenyana na Schalke na Tottenham Hotspur imepewa Borussia Dortmund.
        Kikosi cha Jose Mourinho kinachosuasua kitaanzi nyumbani Uwanja wa Old Trafford kabla ya kusafiri kuwafuata matajiri wa Ufaransa kwa mchezo wa marudiano.


        RATIBA KAMILI HATUA YA 16 BORA YA LIGI YA MABINGWA UKAYA

        Schalke vs Manchester City
        Atletico Madrid vs Juventus
        Manchester United vs PSG
        Tottenham vs Borussia Dortmund 
        Lyon vs Barcelona
        Roma vs Porto 
        Ajax vs Real Madrid
        Liverpool vs Bayern 

        Man City, timu pekee ya England iliyoongoza kundi, itaanzia ugenini kabla ya kucheza nyumbani mechi ya marudiano, lakini timu nyingine zitaanzia ugenini.
        Mechi za kwanza zitachezwa Februari 12, 13, 19 na 20 na za marudiano zitachezwa Machi 5, 6, 12 na 13 mwaka 2019.
        • Blogger Comments
        • Facebook Comments

        0 comments:

        Item Reviewed: MAN UNITED YAPEWA PSG 16 BORA LIGI YA MABINGWA ULAYA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry