• HABARI MPYA

        Sunday, February 28, 2016

        CHEKA ALIVYOHENYESHANA NA MZUNGU HADI KUSHINDA KWA POINTI

        Bondia Francis Cheka wa Tanzania, (kulia) akizuia makonde ya mpinzani wake, Geard Ajetovic Muingereza mwenye asili ya Serbia katika pambano lao la raundi 12 kuwania ubingwa wa Mabara wa WBF uzito wa Super Middle usiku wa kuamkia leo viwanja vya Leaders Club, Kinondoni mjini Dar es Salaam. Cheka alishinda kwa pointi. PICHA ZOTE NA MUHIDDIN SUFIANI WA MAFOTO BLOG 
         Cheka akijitahidi kupangua konde la mpinzani wake....
        Cheka alichanika juu ya jicho la kushoto katika raundi ya nane, lakini akasimama imara na kumaliza pambano
        Cheka akiwa amemtandika ngumi ya mbavuni mpinzani wake
        Cheka akimtupia ngumi mfululizo za kumchagua Geard Ajevotic  
         Cheka alikuwa katkika wakati mgumu jana mbele ya Mserbia huyo anayeshi Uingereza
         Cheka akiinuliwa mkono kutangazwa mshindi baada ya raundi ya 12
        Hapa tayari amevalishwa mkanda wake wa ubingwa wa Mabara wa WBF


        Bondia Cossmas Cheka akivalishwa mkanda wa ubingwa wa WBF Afrika uzito wa Light baada ya kumshinda Mtanzania mwenzake, Mustafa Dotto katika pambano la raundi 12Bondia Mohamed Matumla (kushoto) akimpiga ngumi ya kidevu mpinzani wake, Bakari Mohamed katika pambano lisilo la ubingwa raundi sita uzito wa Light. Matumla alishinda kwa pointi
        • Blogger Comments
        • Facebook Comments

        0 comments:

        Item Reviewed: CHEKA ALIVYOHENYESHANA NA MZUNGU HADI KUSHINDA KWA POINTI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry