// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); YAYA TOURE AMVUA BRAHIMI TUZO YA MWANASOKA BORA AFRIKA WA BBC - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE YAYA TOURE AMVUA BRAHIMI TUZO YA MWANASOKA BORA AFRIKA WA BBC - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Saturday, December 12, 2015

    YAYA TOURE AMVUA BRAHIMI TUZO YA MWANASOKA BORA AFRIKA WA BBC

    KIUNGO wa Ivory Coast na Manchester City, Yaya Toure ameshinda tena Tuzo ya Mwanasoka Bora wa Afrika wa Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) Mwaka 2015, iliyokuwa inashikiliwa na Mualgeria, Yacine Brahimi.
    Nahodha huyo wa Ivory Coast mwenye umri wa miaka 32 anakuwa mchezaji wa tatu, baada ya Wanigeria Nwankwo Kanu na Jay-Jay Okocha, kushinda tuzo hiyo mara mbili.
    Toure amewashinda Yacine Brahimi, Pierre-Emerick Aubameyang, Andre Ayew na Sadio Mane baada ya kura zilizopigwa na mashabiki.
    Mafanikio hayo yanafuatia Toure kuwaongoza Tembo wa Ivory Coast kutwaa Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya miaka 23, hilo likiwa taji lake la kwanza kushinda akiwa na timu ya taifa.
    Yaya Toure ameshinda tena tuzo ya Mwanasoka Bora Afrika

    WASHINDI WA TUZO YA MWANASOKA BORA WA BBC AFRIKA
    2014: Yacine Brahimi (Porto & Algeria)
    2013: Yaya Toure (Manchester City & Ivory Coast)
    2012: Chris Katongo (Henan Construction & Zambia)
    2011: Andre Ayew (Marseille & Ghana)
    2010: Asamoah Gyan (Sunderland & Ghana)
    2009: Didier Drogba (Chelsea & Ivory Coast)
    2008: Mohamed Aboutrika (Al Ahly & MISRI)
    2007: Emmanuel Adebayor (Arsenal & Togo)
    2006: Michael Essien (Chelsea & Ghana)
    2005: Mohamed Barakat (Al Ahly & Misri)
    2004: Jay-Jay Okocha (Bolton & Nigeria)
    2003: Jay-Jay Okocha (Bolton & Nigeria)
    2002: El Hadji Diouf (Liverpool & Senegal)
    2001: Sammy Kuffour (Bayern Munich & Ghana)
    2000: Patrick Mboma (Parma & Cameroon)
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: YAYA TOURE AMVUA BRAHIMI TUZO YA MWANASOKA BORA AFRIKA WA BBC Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top