// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); NAPE NNAUYE NDIYE WAZIRI MPYA WA MICHEZO - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE NAPE NNAUYE NDIYE WAZIRI MPYA WA MICHEZO - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Thursday, December 10, 2015

    NAPE NNAUYE NDIYE WAZIRI MPYA WA MICHEZO

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    MBUNGE wa Mtama, Nape Moses Nnauye ndiye Waziri mpya wa Utamaduni, Sanaa na Michezo.
    Akitangaza Baraza la Mawaziri leo Ikulu mjini Dar es Salaam, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Pombe Joseph Magufuli amesema Katibu huyo Mwenezi wa CCM hatakuwa na Naibu.
    Awali, Wizara hiyo ilikuwa inajulikana kama Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo chini Dk Fenella Mukangara, ambaye Naibu wake alikuwa Amos Makala na baadaye Juma Nkamia. 
    Nape Nnauye ndiye Waziri mpya wa Michezo Tanzania
     

    Rais Magufuli amesema atakuwa na Mawaziri 19 na kwamba baadhi ya Wizara zitakuwa na Mawaziri na hazitakuwa na Manaibu Waziri, lengo ni kuwa na baraza dogo kupunguza gharama. “Zilitengwa Sh. bilioni 2, Mawaziri watakapoteuliwa waende semina elekezi, baraza nitakaloliteua halitakuwa na semina elekezi na fedha tutaelekeza sehemu nyingine kama ni madawati au kwenye elimu bure,”amesema.

    BARAZA KAMILI LILILOTANGAZWA NI;
    Tamisemi, Utumishi na Utawala Bora; Simbachawene na Angela Kairuki 
    Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora; Mawaziri wawili ambao ni Mh. Simbachawene na Kairuki
    Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu; Waziri Jenista Mhagama, Naibu waziri Dk. Possy Abdallah.
    Wizara ya Mambo ya Nje na EAC/ Kimataifa; Augustino Mahiga, Naibu Waziri - Dk. Suzan Kolimba
    Wizara ya Ardhi, Nyumba na Makazi; Waziri wake ni William Lukuvi na Naibu wake ni Angelina Mabula
    Wizara ya Elimu; Waziri bado hajapatikana, Naibu Stella Manyanya
    Wizara ya Afya Jinsia na Watoto: Ummy Mwalimu, Naibu wake Kigwangalla
    Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi; Waziri: Mwigulu Nchemba Naibu Waziri: William Tate Ole Nashon
    Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano; Waziri bado hajapatikana,Naibu waziri Eng.Edwin Amandus Ngonyani.
    Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye
    Wizara ya Fedha na Mipango; Waziri bado hajapatikana, Naibu Waziri wake ni Dk. Ashantu Kijachi.
    Ofisi ya Makamu wa Rais/Muungano na Mazingira; Waziri January Makamba,Naibu waziri Luhaga Mpina.
    Wizara ya Nishati na Madini; Waziri ni Sospeter Muhongo na Naibu Waziri wake ni Medard Kalemani.
    Wizara ya Katiba na Sheria; Waziri ni Harrison Mwakyembe
    Wizara ya Mambo ya Nje,Afrika Mashariki Kikanda na Kimataifa; Waziri ni Augustine Mahiga N/Waziri Susan Kolimba
    Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa; Waziri ni Husein Mwinyi
    Wizara ya Mambo ya Ndani; Waziri ni Charles Kitwanga.
    Wizara ya Sayansi, Teknolojia, Elimu na Ufundi; Waziri bado hajapatikana na Naibu Waziri wake ni Stela Manyanya.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NAPE NNAUYE NDIYE WAZIRI MPYA WA MICHEZO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top