// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); STEWART HALL: MBIO ZA UBNGWA SASA ZIMESHIKA KASI AZAM FC - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE STEWART HALL: MBIO ZA UBNGWA SASA ZIMESHIKA KASI AZAM FC - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

        Friday, October 30, 2015

        STEWART HALL: MBIO ZA UBNGWA SASA ZIMESHIKA KASI AZAM FC

        MECHI ZIJAZO LIGI KUU YA VODACOM TZ BARA
        Oktoba 31, 2015
        Simba SC Vs Majimaji FC
        Kagera Sugar Vs Yanga SC
        Mtibwa Sugar Vs Mwadui FC
        Prisons Vs Ndanda FC
        Coastal Union Vs Mbeya City
        Novemba 1, 2015
        African Sports Vs JKT Ruvu
        Azam FC Vs Toto Africans
        Novemba 2, 2015
        Mgambo Shooting Vs Stand United
        Kocha Muingereza wa Azam FC, Stewart Hall amesema mbio za ubingwa sasa zimeshika kasi katika timu yake

        Na Princess Asia,  DAR ES SALAAM
        KOCHA Mkuu Azam FC, Muingereza Stewart John Hall amesema kwamba anataka kuendeleza wimbi la ushindi ili kuhakikisha anatimiza ndoto za kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
        Azam FC jana imepanda kileleni kwa Ligi Kuu kufuatia ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya JKT Ruvu, Uwanja wa Karume, Dar es Salaam, hivyo kufikisha pointi 22, mbili zaidi ya mabingwa watetezi, Yanga SC, baada ya timu zote hizo kucheza mechi nane.
        Akizungumza na BIN ZUBEIRY SPORTS- ONLINE jana, kocha huyo aliyeipa Azam FC ubingwa wa Afrika Mashariki, Kombe la Kagame Agosti mwaka huu, amesema kwamba lengo si kuwa kileleni mwa Ligi Kuu kwa muda, bali kutwaa ubingwa.
        “Si suala la kuwa juu tu, nataka kufikia malengo tuliyojiwekea, hivyo kazi kubwa iliyopo mbele yetu ni kuhakikisha tunapata pointi tatu za kila mechi tutakazocheza,” alisema.
        John Bocco jana amefunga mabao mawili katika ushindi wa 4-2 wa Azam FC

        Stewart amefurahishwa na safu yake ya ushambuliaji kwa kucheza kwa ‘njaa ya kufunga’ na kufuata maelekezo anayowapa kabla ya mchezo.
        “Nina imani na safu yangu ya ushambuliaji, kama bao la nne lililofungwa na Kipre Tchetche ni la aina yake, ile ilikuwa moja ya maagizo niliyomuagiza na kufanyia kazi,” amesema.
        Azam FC inatarajiwa kushuka tena dimbani Jumapili kumenyana na Toto Africans katika mfululizo wa ligi hiyo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
        Kwa ujumla Ligi Kuu inaendelea mwishoni mwa wiki, Jumamosi Simba SC ikimenyana na Majimaji FC Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Yanga SC na Kagera Sugar Uwanja wa Mwinyi, Tabora, Mtibwa Sugar na Mwadui FC Uwanja wa Manungu, Turiani, Morogoro, Prisons na Ndanda FC Uwanja wa Sokoine, Mbeya na Coastal Union na Mbeya City Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.
        Mechi nyingine zitachezwa Jumapili, na mbali ya Azam FC na Toto, Uwanja wa Mkwakwani, Tanga African Sports itakuwa mwenyeji wa JKT Ruvu wakati Jumatatu, Mgambo Shooting itaikaribisha Stand United Uwanja wa Mkwakwani.
        • Blogger Comments
        • Facebook Comments

        0 comments:

        Item Reviewed: STEWART HALL: MBIO ZA UBNGWA SASA ZIMESHIKA KASI AZAM FC Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry