// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); DIAMOND ALITEKA JIJI LA DAR, MAMIA WAJITOKEZA KUMPOKEA NA TUZO ZAKE - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE DIAMOND ALITEKA JIJI LA DAR, MAMIA WAJITOKEZA KUMPOKEA NA TUZO ZAKE - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Thursday, October 15, 2015

    DIAMOND ALITEKA JIJI LA DAR, MAMIA WAJITOKEZA KUMPOKEA NA TUZO ZAKE

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    MASHABIKI wa Msanii anayetamba hapa nchini katika Anga ya muziki wa kizazi kipya Naseeb Abdul ‘Diamond Platinumz’ jana walifunga barabara ya kutoka Uwanja wa Ndege kwa muda wakati Msanii huyo alipowasili.
    Diamond aliwasili Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere jana akitokea Nchini Marekani alikotwaa tuzo tatu za Afrimma wikiendi ya wiki iliyopita huku akipata mapokezi ya aina yake.
    Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwasili Uwanjani hapo Diamond alisema, atahakikisha hawaangushi mashabiki wake wanaochangia kwa asilimia kubwa kupata tuzo hizo.
    Diamond Platinumz akionyesha tuzo zake wakati wa maandamazo ya mapokezi yake leo

    Nyota huyo asiyekuwa na mpinzani kwa sasa hapa nchini, alisema kwake yeye ni faraja kubwa, kuona Tanzania inatambulika kupitia yeye, hivyo inampa nafasi ya kuzidi kupambana zaidi na kuitangaza kwani anatambua ana deni kubwa la kuhakikisha anafanya vizuri.
    Mara baada ya kuzungumza na wanahabari, Masgabiki hao walianza msafara wakiwa naye na kupelekea kusababisha msongamano mkubwa ulioziba njia kutokana na matembezi hayo.
    Diamond akiwa katikati ya umati wa watu

    Mashabiki hao wakiongozwa na kundi lake la Wasafi walianza kuongozana na Diamond wakitembea katikati ya barabara kitendo kilichofanya msongamano mkubwa uliowaradhimu Polisi kuingilia kati.
    Baada ya kufika eneo la Vingunguti kwa mguu, baada ya Polisi kufika walimtaka Diamond kusitisha maandamano hayo kwa kupanda gari ili kuepusha msongamano huo, baada ya taarifa hiyo ya Polisi ilimradhimu Diamond kupanda gari la Grobal Publishers huku wafuasi wake wengine wakipanda pikipiki.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: DIAMOND ALITEKA JIJI LA DAR, MAMIA WAJITOKEZA KUMPOKEA NA TUZO ZAKE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top