BONDIA Tyson Fury ametamba atamaliza zama za utawala wa Wladimir Klitschko katika ndondi za uzito wa juu katika pambano lao la Oktoba 24, mwaka huu.
"Nawaambia watu wa Uingereza nitamaliza zama za Klitschko. Wote wa Ulaya wanataka mimi nimpige. Kwa muda mrefu Wladimir na kaka yake, Vitali wamezipoozesha ndondi kwa staili ya ngumi zao za kuboa. Mimi ni damu mpya ya ngumi za uzito wa juu na nitammaliza na kuwa bingwa mpya wa dunia,".
Pambano la Klitschko vs Fury litakalofanyika Oktoba 24, mwaka huu siku ambayo Kell Brook wa Sheffield atatetea mkanda wake wa dunia wa uzito wa Welter dhidi ya Diego Chaves, litaonyeshwa na Televisheni ya Sky.
0 comments:
Post a Comment