KOCHA wa zamani wa Yanga SC, Mbelgimji Tom Saintfiet ameiwezesha Togo kushinda mechi ya pili mfululizo kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Mataifa ya Afrika baada ya jana kuifunga 2-0 Djibouti.
Togo ambayo ilimkosa nyota wake, Emmanuel Adebayor aliyekataa kujiunga na timu baada ya kupokonywa Unahodha katika mchezo uliopita wakishinda 2-1 dhidi ya Liberia mweziu June.
Nahodha mpya, Serge Akakpo aliifungia bao la kwanza Togo dakika ya tatu kabla ya Jonathan Ayite kufunga la pili kipindi chakwanza na sasa Togo inaongoza Kundi A kwa pointi zake sita.
Mechi nyingine ya kundi hilo leo Tunisia watamenyana na Liberia. Huo utakuwa mchezo wa kwanza kuchezwa mjini Monrovia tangu ufungiwe kutokana na tishio la ugonjwa wa Ebola.
Tunisia iliifunga 8-1 Djibouti katika mchezo wa kwanza wa kundi hilo Juni.
Togo ambayo ilimkosa nyota wake, Emmanuel Adebayor aliyekataa kujiunga na timu baada ya kupokonywa Unahodha katika mchezo uliopita wakishinda 2-1 dhidi ya Liberia mweziu June.
Nahodha mpya, Serge Akakpo aliifungia bao la kwanza Togo dakika ya tatu kabla ya Jonathan Ayite kufunga la pili kipindi chakwanza na sasa Togo inaongoza Kundi A kwa pointi zake sita.
Mechi nyingine ya kundi hilo leo Tunisia watamenyana na Liberia. Huo utakuwa mchezo wa kwanza kuchezwa mjini Monrovia tangu ufungiwe kutokana na tishio la ugonjwa wa Ebola.
Tunisia iliifunga 8-1 Djibouti katika mchezo wa kwanza wa kundi hilo Juni.
0 comments:
Post a Comment