KLABU ya Manchester United imemuorodhesha kipa wa zamani wa Barcelona, Victor Valdes katika kikosi chake cha wachezaji 25 watakaocheza Ligi Kuu ya England.
Valdes ametengwa na kocha Louis Van Gaal baada ya mwalimu huyo kudai kwamba mlinda mlango huyo aligoma kuchezea timu ya vijana chini ya umri wa miaka 21 jambo ambalo lilimfanya atemwe kwenye ziara ya kujiandaa na msimu nchini Marekani.
Tangu hapo, kipa huyo mwenye umri wa miaka 33 amekuwa akifanya mazoezi kivyake na alitarajiwa kusaini Besiktas mwishoni mwa wiki, lakini akiwa hoteli ya Uwanja wa Ndege wa Manchester tayari kwa safari ya kwenda kukamilisha uhamisho wake, dili likabuma na dirisha likafungwa.
0 comments:
Post a Comment