// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); TP MAZEMBE YASAJILI BEKI LA SANGA BALENDE - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE TP MAZEMBE YASAJILI BEKI LA SANGA BALENDE - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Friday, August 07, 2015

    TP MAZEMBE YASAJILI BEKI LA SANGA BALENDE

    KLABU ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya KOngo (DRC) imemsajili beki wa kati anayeweza kucheza kama kiungo pia, Badibake Mpongo.
    Mchezaji huyo wa Sanga Balende amesaini Mkataba wa miaka mitatu kuhamia kwa mabingwa wa DRC, baada ya klabu yake kumalizana na Mazembe. 
    Na huyo anakuwa mchezaji wa tatu kusajiliwa na mabingwa wa Ligi Kuu ya DRC ambao kikosi wana Watanzania wawili, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu.
    Badiabake Mpongo kulia ametua TP Mazembe

    Mazembe inaimarisha kikosi chake kuelekea msimu ujao wa Ligi Kuu ya DRC maarufu kama Linafoot na klabu imefurahia ujio wa mchezaji huyo ‘fundi’.
    Kwa upande wake, Mpongo amesema; “Ni heshima kubwa kwangu kujiunga na TPM, klabu ambayo ni faraja ya nchi. Sasa naelekeza fikra zangu katika kucheza na kushinda mataji hapa,”amesema Badibake Mpongo, ambaye tayari ameanza mazoei na The Ravens. 

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TP MAZEMBE YASAJILI BEKI LA SANGA BALENDE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top