Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
KIUNGO Amri Ramadhani Kiemba ameondoka leo Dar es Salaam kwenda Addis Ababa, Ethiopia kuungana na timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars kwa safari ya Misri.
Taifa Stars inakwenda Misri baadaye leo kwa ajili a mchezo wa kwanza wa Kundi G kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika 2017 nchini Gabon dhidi ya Misri.
Kiemba alikuwa katika kikosi cha pili cha timu ya taifa, chini ya kocha Salum Mayanga ambacho kilikwenda Rwanda kwa mchezo wa kirafiki dhidi ya wenyeji, wakati Taifa Stars A inakwenda kambini Ethiopia.
Na kocha wa Taifa Stars, Mart Nooij amelazimika kumuita Kiemba baada ya kumkosa kiungo mshambuliaji, Mrisho Khalfan Ngassa ambaye ametingwa na shughuli binafsi.
Kwa mujibu wa Mkuu wa Msafara wa Taifa Stars, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ maandalizi ya timu ni mazuri na kuna matumaini makubwa ya ushindi wa ugenini.
“Kwa kweli maandalizi yetu hapa Addis yamekuwa mazuri sana, vijana wamefanya mazoezi katika mazingira mazuri na wapo vizuri kabisa. Ni kwamba tuna matumaini makubwa ya ushindi wa ugenini,”amesema Kaburu.
KIUNGO Amri Ramadhani Kiemba ameondoka leo Dar es Salaam kwenda Addis Ababa, Ethiopia kuungana na timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars kwa safari ya Misri.
Taifa Stars inakwenda Misri baadaye leo kwa ajili a mchezo wa kwanza wa Kundi G kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika 2017 nchini Gabon dhidi ya Misri.
Kiemba alikuwa katika kikosi cha pili cha timu ya taifa, chini ya kocha Salum Mayanga ambacho kilikwenda Rwanda kwa mchezo wa kirafiki dhidi ya wenyeji, wakati Taifa Stars A inakwenda kambini Ethiopia.
Na kocha wa Taifa Stars, Mart Nooij amelazimika kumuita Kiemba baada ya kumkosa kiungo mshambuliaji, Mrisho Khalfan Ngassa ambaye ametingwa na shughuli binafsi.
Kwa mujibu wa Mkuu wa Msafara wa Taifa Stars, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ maandalizi ya timu ni mazuri na kuna matumaini makubwa ya ushindi wa ugenini.
“Kwa kweli maandalizi yetu hapa Addis yamekuwa mazuri sana, vijana wamefanya mazoezi katika mazingira mazuri na wapo vizuri kabisa. Ni kwamba tuna matumaini makubwa ya ushindi wa ugenini,”amesema Kaburu.
![]() |
Amri Kiemba akiwa Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam leo kwa safari ya Addis Ababa |
0 comments:
Post a Comment