// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); MANYIKA MDOGO AFIKISHA MECHI 20 SIMBA SC, AMEFUNGWA MABAO 14 TU - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE MANYIKA MDOGO AFIKISHA MECHI 20 SIMBA SC, AMEFUNGWA MABAO 14 TU - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

        Tuesday, April 07, 2015

        MANYIKA MDOGO AFIKISHA MECHI 20 SIMBA SC, AMEFUNGWA MABAO 14 TU

        Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
        KIPA ‘bwana mdogo’ Peter Manyika Jr. jana amedaka mechi ya 20 msimu huu katika klabu yake, Simba SC jambo ambalo ni kinyume kabisa cha matarajio.
        Simba SC imeshinda 2-1 dhidi ya wenyeji wa kuhamia, Kagera Sugar ya Bukoba Uwanja wa Kambarage, Shinyanga katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.  
        Manyika alisajiliwa kama kipa wa tatu Simba SC, tena akiorodheshwa kwenye kikosi cha vijana, ‘Simba B’, lakini akalazimika kuanza kazi mapema baada ya makipa wote wa juu yake kuwa majeruhi. 
        Peter Manyika Jr. jana amedaka mechi ya 20 Simba SC, akifungwa bao la 14

        Septemba mwaka jana Simba SC ilikwenda Afrika Kusini na makipa wawili, Hussein Sharrif ‘Casillas’ na Manyika kutokana na Ivo Mapunda kuumia kidole.
        Lakini kwa bahati mbaya zaidi, Casillas naye akaumia ugoko akiidakia timu hiyo mchezo wa kirafiki dhidi ya Orlando Pirates, hivyo Manyika kuingia dakika ya 43 kumalizia mchezo.
        Casillas hajaweza kurejea langoni tangu hapo na Manyika amekuwa akipokezana na Ivo kudaka, jana akifikisha mechi 20, akiwa amefungwa mabao 14 tu katika mechi zote hizo.
        Tayari Manyika ni kipa wa kuaminiwa Simba SC licha ya umri wake mdogo- jambo ambalo linamtengenezea mazingira mazuri ya kuwa kipa bora baadaye.
        Manyika ambaye amerithi kazi hiyo kutoka kwa baba yake mzazi, Manyika Peter Sr., anaelekea kufuata vyema nyayo za mzazi wake huyo, kwani tayari amepandishwa kikosi cha timu ya pili ya taifa, maarufu kama Taifa Stars Maboresho ambako alisimama langoni kwa dakika zote 90 katika sare ya 1-1 na Rwanda Januari 22, mwaka huu. 
        Manyika Sr aliwika katika klabu za Mtibwa Sugar, Yanga SC na timu ya taifa, Taifa Stars kabla ya kustaafu na kuwa kocha wa makipa, huku pia akifanya muziki.
        Wakati Manyika Jr. amedaka mechi 20 katika msimu wake wa kwanza Simba SC na kufungwa mabao 14, Ivo ambaye anamaliza Mkataba wake wa mwaka mmoja na nusu Juni mwaka juu, tangu atue Msimbazi Desemba mwaka juzi, amedaka mechi 36 na kufungwa mabao 24.
        Casillas naye ambaye amesajiliwa msimu huu kutoka Mtibwa Sugar, yeye hadi anaumia Oktoba mwaka jana alikuwa amedaka mechi nane na kufungwa mabao manne.

        REKODI YA PETER MANYIKA JR. SIMBA SC

        Simba SC 0-0 Orlando Pirates (kirafiki aliingia dk43 hakufungwa, Afrika Kusini) 
        Simba SC 2-4 Bidvest Witss (Kirafiki, alifungwa nne Afrika Kusini) 
        Simba SC 0-2 Jomo Cossmos (Kirafiki, alifungwa mbili Afrika Kusini) 
        Simba SC 0-0 Yanga SC (Ligi Kuu, hakufungwa)
        Simba SC 1-1 Prisons (Ligi Kuu, alifungwa moja)
        Simba SC 1-1 Mtibwa Sugar (Ligi Kuu, aliokoa penalty, akafungwa moja)
        Simba SC 0-0 Express (Kirafiki, hakufungwa) 
        Simba SC 0-1 Mtibwa Sugar (Kombe la Mapinduzi, Zanzibar alifungwa moja)
        Simba SC 1-0 Mafunzo (Kombe la Mapinduzi, Zanzibar hakufungwa)
        Simba SC 1-0 JKU (Kombe la Mapinduzi, hakufungwa)
        Simba SC 4-0 Taifa Jang’ombe (Robo Fainali Kombe la Mapinduzi, hakufungwa)
        Simba SC 1-0  Polisi (Nusu Fainali Kombe la Mapinduzi, hakufungwa)
        Simba SC 0-0  Mtibwa Sugar (Alimpisha Ivo dakika ya 90, Simba ikashinda penalti 4-3 Fainali Kombe la Mapinduzi)
        Simba SC 2-0 Ndanda FC (Ligi Kuu Mtwara, hakufungwa)
        Simba SC 1-1 Azam FC (Ligi Kuu, alifungwa moja) 
        Simba SC 1-2 Mbeya City (Ligi Kuu Taifa, alifungwa mbili)
        Simba SC 2-0 Polisi Moro (Ligi Kuu, aliingia kipindi cha kwanza kumalizia baada ya Ivo kuumia, hakufungwa) 
        Simba SC 0-2 Mgambo Shooting (Ligi Kuu, alifungwa moja baada ya kuingia kuchukua nafasi ya Ivo aliyetolewa kwa kadi nyekundu kipindi cha pili)
        Simba SC 3-0 Ruvu Shooting (Ligi Kuu, hakufungwa)
        Simba SC 2-1 Kagera Sugar (Ligi Kuu, aliungwa moja)
        Manyika Peter Sr. kwa sasa ni kocha wa makipa, baada ya kuwika Yanga na Taifa Stars enzi zake
        • Blogger Comments
        • Facebook Comments

        0 comments:

        Item Reviewed: MANYIKA MDOGO AFIKISHA MECHI 20 SIMBA SC, AMEFUNGWA MABAO 14 TU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry