Na Prince Akbar, DAR ES SALAAM
HALI ya kiungo mshambuliaji wa Yanga SC, Mbrazil Andrey Coutinho inazidi kuimarika taratibu na bila shaka hadi mchezo dhidi ya Etoile du Sahel, atakuwa fiti kwa asilimia 100.
Yanga SC itakutana na Etoile du Sahel ya Tunisia katika hatua ya 16 Bora Kombe la Shirikisho Afrika katikati ya mwezi huu mjini Dar es Salaam kabla ya kurudiana wiki mbili baadaye Tunis.
Na Coutinho ambaye hajacheza mpira mwezi wote uliopita kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya goti baada ya kuumia akiichezea timu hiyo mjini Mbeya, anatarajiwa kuwa fiti kabisa.
Coutinho ameanza programu kamili ya mazoezi Yanga SC na yeye mwenyewe amesema anafurahishwa na jinsi hali yake inavyoendelea.
“Ninaendelea vizuri, natumaini baada ya mechi mbili nitakuwa katika ubora wangu kabisa. Hata sasa najisikia vizuri kabisa na nina hamu ya kucheza tena,”amesema.
HALI ya kiungo mshambuliaji wa Yanga SC, Mbrazil Andrey Coutinho inazidi kuimarika taratibu na bila shaka hadi mchezo dhidi ya Etoile du Sahel, atakuwa fiti kwa asilimia 100.
Yanga SC itakutana na Etoile du Sahel ya Tunisia katika hatua ya 16 Bora Kombe la Shirikisho Afrika katikati ya mwezi huu mjini Dar es Salaam kabla ya kurudiana wiki mbili baadaye Tunis.
Na Coutinho ambaye hajacheza mpira mwezi wote uliopita kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya goti baada ya kuumia akiichezea timu hiyo mjini Mbeya, anatarajiwa kuwa fiti kabisa.
![]() |
Andrey Coutinho kushoto sasa anafanya mazoezi kikamilifu Yanga SC |
Coutinho ameanza programu kamili ya mazoezi Yanga SC na yeye mwenyewe amesema anafurahishwa na jinsi hali yake inavyoendelea.
“Ninaendelea vizuri, natumaini baada ya mechi mbili nitakuwa katika ubora wangu kabisa. Hata sasa najisikia vizuri kabisa na nina hamu ya kucheza tena,”amesema.
0 comments:
Post a Comment