Na Vincent Malouda, NAIROBI
BANDARI FC wamemaliza pasaka yao na kichapo cha magoli 2-0 na Ulinzi Stars kwenye mechi ya ligi kuu Kenya, KPL, iliyogaragazwa ugani Mbaraki alasiri ya leo.
John Makwata aliipa Ulinzi bao la kwanza dakika ya 53 akimalizia krosi murwa yake Oliver Ruto aliyetokezea pembeni kisha Oscar Wamalwa akapigilia msumari wa mwisho kwenye jeneza la Bandari dakika ya 60. Chipukizi huyo alitumia uzembe wa mabeki Shariff Mohammed na Humphrey Okot wa kutoondoa uchafu langoni kwa kuwachilia pande la shuti hadi nyavuni kipa Wilson Obungu akibakia kuhesabu ndege baharini.
Mbinu za vijana wa Twahir Muhiddin kuhifadhi rekodi yao ya kutopoteza ngarambe yoyote nyumbani hazikufua dafu David King'atua, Mganda George Abege na Victor Ndinya wakipoteza nafasi za kuhesabu.
Katika matokeo ya wikiendi, Jesse Were alicheka na nyavu mara mbili na kuinusuru Tusker FC kutoka kwa mtego wa Chemelil Sugar Jumamosi ugani Chemelil Sports Complex. Hamisi Mwinyi na Daniel Mutahi walikuwa wameiweka Chemelil kifua mbele.
Kwingineko siku ya jumapili, Western Stima waliibuka washindi dhidi ya Sofapaka kwao Kisumu kwa magoli 3-2, Mathare United 2-0 City Stars, Muhoroni Youth 1-1 Ushuru FC, Nakuru AllStars 1-0 SoNy Sugar huku Thika United ikivuna pointi moja dhidi ya mabingwa mara 12 AFC Leopards katika uchanjaa wa Mumias.
Ni Jumapili iyo iyo mabingwa watetezi Gor Mahia waliondolewa katika mechi za mabingwa barani Afrika na AC Leopard ya Congo magoli 2-0 kwa jumla baada ya 1-0 mjini Dolisie.
Mechi za ligi kuu ya Shirikisho la Soka Kenya, FKF PL, vile vile zilisakatwa wikiendi iliyopita na haya ndio matokeo yake.
Jumamosi
Kakamega Homeboyz 0-0 Kariobangi Sharks
FC Talanta 1-2 Zoo Kericho
Oserian 2-0 St. Joseph
Moyas 0-2 Ligi Ndogo
Nzoia United 1-1 Shabana FC
Jumapili
Nairobi Stima 0-3 Bidco United
Posta Rangers 2-0 Agrochemicals
West Kenya 2-1 Finlays Horticulture
BANDARI FC wamemaliza pasaka yao na kichapo cha magoli 2-0 na Ulinzi Stars kwenye mechi ya ligi kuu Kenya, KPL, iliyogaragazwa ugani Mbaraki alasiri ya leo.
John Makwata aliipa Ulinzi bao la kwanza dakika ya 53 akimalizia krosi murwa yake Oliver Ruto aliyetokezea pembeni kisha Oscar Wamalwa akapigilia msumari wa mwisho kwenye jeneza la Bandari dakika ya 60. Chipukizi huyo alitumia uzembe wa mabeki Shariff Mohammed na Humphrey Okot wa kutoondoa uchafu langoni kwa kuwachilia pande la shuti hadi nyavuni kipa Wilson Obungu akibakia kuhesabu ndege baharini.
Mbinu za vijana wa Twahir Muhiddin kuhifadhi rekodi yao ya kutopoteza ngarambe yoyote nyumbani hazikufua dafu David King'atua, Mganda George Abege na Victor Ndinya wakipoteza nafasi za kuhesabu.
Katika matokeo ya wikiendi, Jesse Were alicheka na nyavu mara mbili na kuinusuru Tusker FC kutoka kwa mtego wa Chemelil Sugar Jumamosi ugani Chemelil Sports Complex. Hamisi Mwinyi na Daniel Mutahi walikuwa wameiweka Chemelil kifua mbele.
Kwingineko siku ya jumapili, Western Stima waliibuka washindi dhidi ya Sofapaka kwao Kisumu kwa magoli 3-2, Mathare United 2-0 City Stars, Muhoroni Youth 1-1 Ushuru FC, Nakuru AllStars 1-0 SoNy Sugar huku Thika United ikivuna pointi moja dhidi ya mabingwa mara 12 AFC Leopards katika uchanjaa wa Mumias.
Ni Jumapili iyo iyo mabingwa watetezi Gor Mahia waliondolewa katika mechi za mabingwa barani Afrika na AC Leopard ya Congo magoli 2-0 kwa jumla baada ya 1-0 mjini Dolisie.
Mechi za ligi kuu ya Shirikisho la Soka Kenya, FKF PL, vile vile zilisakatwa wikiendi iliyopita na haya ndio matokeo yake.
Jumamosi
Kakamega Homeboyz 0-0 Kariobangi Sharks
FC Talanta 1-2 Zoo Kericho
Oserian 2-0 St. Joseph
Moyas 0-2 Ligi Ndogo
Nzoia United 1-1 Shabana FC
Jumapili
Nairobi Stima 0-3 Bidco United
Posta Rangers 2-0 Agrochemicals
West Kenya 2-1 Finlays Horticulture
0 comments:
Post a Comment