// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); RED ARROWS FC KUWEKA KAMBI TANZANIA. - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE RED ARROWS FC KUWEKA KAMBI TANZANIA. - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Thursday, February 12, 2015

    RED ARROWS FC KUWEKA KAMBI TANZANIA.

    Na Baraka Kizuguto, DAR ES SALAAM
    KLABU ya Red Arrow FC inayoshiriki Ligi Kuu nchini Zambia inatarajiwa kuwasili jijini Dar es salaam-Tanzania Jumatatu ya wiki ijayo kwa ajili ya kuweka kambi ya mafunzo ya wiki moja kujindaa na msimu mpya wa Ligi Kuu nchini humo 2015.
    Uongozi wa klabu hiyo chini ya mwenyekiti wake Col Nolacso K Chilando ulifika leo makao makuu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Tanzania - TFF sambamba na Ofisa Habari wa klabu, Luteni Kanali Melody Siisii, Alex Chila Ofisa ubalozi wa Zambia nchini Tanzania kujitambulisha uwepo wao nchini.

    Kutoka kushoto ni Ofisa habari wa Red Arrows  Lt Melody Siisii, Mwenyekiti wa Red Arrows Col Nolasco Chilando, Katibu Mkuu wa TFF Selestine Mwesigwa na Ofisa Ubalozi wa Zambia nchini Tanzania Alex Chila, wakiwa ofisi za TFF - PPF Tower leo.

    Wakiongea na katibu  mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Selestine Mweisgwa, uongozi wa timu hiyo umesema maandalizi ya kambi yameshakamilika na kikubwa walikua wanaliomba Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini kutambua uwepo wao na kuwasaidia kupata viwanja vya kufanyia mazoezi.
    Naye Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini -TFF Bw.Mwesigwa  alisema wameyapokea maombi hayo ya Red Arrow FC  na kuwakaribisha nchini kwa ajili ya kambi yao na kusema ujio wao utafungua milango kwa vilabu vingine pia kuja kuweka kambi nchini.
    Timu ya Red Arrow FC inayomilikiwa na jeshi la Anga nchini Zambia ikiwa nchini kwa mafunzo, inatarajia kucheza mchezo mmoja wa kirafiki na imeliomba Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini kuwatafutia timu moja ya kucheza nayo.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RED ARROWS FC KUWEKA KAMBI TANZANIA. Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top