// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); STAND UNITED YAWAFUMUA 4-1 MIGAMBO, MTIBWA NA MBEYA CITY ZATULIZWA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE STAND UNITED YAWAFUMUA 4-1 MIGAMBO, MTIBWA NA MBEYA CITY ZATULIZWA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Saturday, February 14, 2015

    STAND UNITED YAWAFUMUA 4-1 MIGAMBO, MTIBWA NA MBEYA CITY ZATULIZWA

    TIMU ya Stand United imeichapa mabao 4-1 Mgambo Shooting katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Kambarage Shinyanga.
    Ushindi huo unakuja siku chache baada ya wachezaji wa timu hiyo kupewa mafundisho na kocha Msaidizi wa timu ya taifa ya Uholanzi, Patrick Kluivert.
    Mshambuliaji huyo wa zamani wa Barcelona alizuru Shinyanga wiki hii kufungua cha soka cha watoto katika sekondari ya Com na akapata fursa ya kuhudhuria mazoezi ya Stand United Uwanja wa Kambarage na kuwapa mawaidha.

    Katika mechi nyingine za Ligi Kuu leo, Mbeya City imelazimishwa sare ya bila kufungana na wenyeji Coastal Union Uwanja wa Mkwakwani, Tanga wakati Mtibwa Sugar nayo imetoka 0-0 na wenyeji Ndanda, Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara.     
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: STAND UNITED YAWAFUMUA 4-1 MIGAMBO, MTIBWA NA MBEYA CITY ZATULIZWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top