// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); KOLO TOURE ASTAAFU SOKA YA KIMATAIFA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE KOLO TOURE ASTAAFU SOKA YA KIMATAIFA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Sunday, February 15, 2015

    KOLO TOURE ASTAAFU SOKA YA KIMATAIFA

    BEKI wa Liverpool na Ivory Coast, Kolo Toure ametangaza kustaafu soka ya kimataifa baada ya kuitumikia Tembo kwa miaka 15.
    Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 33 amecheza Fainali tatu za Kombe la Dunia na saba za Kombe la Mataifa ya Afrika tangu aanze kucheza timu ya taifa mwaka 2000.
    Baada ya kufungwa katika katika fainali mbili za AFCON, hatimaye Kolo alitimiza ndoto zake za kuinua ndoo ya Mataifa ya Afrika baada ya Ivory Coast kuishinda Ghana kwa matuta michuano ya mwaka 2015, wiki iliyopita nchini Equatorial Guinea.
    Ivory Coast's defender Kolo Toure raises the trophy as he celebrates winning the 2015 African Cup of Nations
    Beki wa Ivory Coast, Kolo Toure akifurahia na Kombe la Mataifa ya Afrika wiki iliyopita baada ya kuifunga Ghana kwa penalti 9-8 kufuatia sare ya 0-0 ndani ya dakika 120 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KOLO TOURE ASTAAFU SOKA YA KIMATAIFA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top