// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); GOR MAHIA WAITWANGA SOFAPAKA NA KUBEBA ‘SUPER CUP’ YA KENYA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE GOR MAHIA WAITWANGA SOFAPAKA NA KUBEBA ‘SUPER CUP’ YA KENYA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Wednesday, February 11, 2015

    GOR MAHIA WAITWANGA SOFAPAKA NA KUBEBA ‘SUPER CUP’ YA KENYA

    Na Mahmoud Zubeiry, NAIROBI
    MABINGWA wa Kenya, Gor Mahia usiku huu wametwaa taji la DSTV Super Cup, mechi maalum ya kuashiria kupenuliwa kwa pazia la Ligi Kuu ya Kenya, baada ya kuifunga mabao 2-1 Sofapaka Uwanja wa Nyayo, Nairobi.
    Kwa ushindi huo, Gor inayofundishwa na kocha Mscotland, Frank Nuttal imezawadiwa fedha za Kenya, Sh. Milioni 1, zaidi ya Sh. Milioni 14 za Tanzania, wakati mabingwa wa Ngao ya GOtv, Sofapaka wamepatiwa Sh 500,000 za Kenya.
    Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Moses Osano, hadi mapumziko, tayari Gor- mabingwa mara nyingi zaidi Ligi Kuu Kenya, (14) tayari walikuwa mbele kwa bao 1-0, lililofungwa na Victor Ally Abondo.
    Abondo alifunga bao hilo dakika ya 20 akiupitisha mpira juu ya kipa, David Okello kufuatia krosi ya Mganda, Khalid Aucho.
    Mkuu wa SuperSport Afrika, Andre Venter akimkabidhi Kombe la DSTV Super Cup, nahodha wa Gor Mahia, Victor Ally Abondo kulia usiku huu Uwanja wa Nyayo


    Sofapaka inayofundishwa na kocha Mganda, Sam Timbe, ilipambana kurudisha bao hilo kipindi cha kwanza bila na mafanikio.
    Kipindi cha pili, nyota ya Gor Mahia iliendelea kung’ara baada ya kufanikiwa kupata bao la pili dakika ya 68, mfungaji Abondo tena kwa mkwaju wa penalti, baada ya Michael Olunga kuangushwa kwenye eneo la hatari na kipa Okello.
    Zikiwa zimesalia dakika mbili mchezo kumalizika, kiungo wa Gor Mahia, Mganda Innocent Wafula alimfunga kipa wake, Boniface Oluoch wakati akiondoa mpira kwenye himaya ya mshambuliaji wa Sofapaka, Enock Agwanda.
    Kwa ujumla, Gor walistahili ushindi wa leo, kutokana na kucheza vizuri kuliko wapinzani wao.
    Ligi Kuu ya Kenya inatarajiwa kuanza mwishoni mwa wiki, ingawa Gor na Sofapaka zote zitakuwa kwenye michuano ya Afrika.       
    Hata hivyo, bado kiza kimetanda katika soka ya Kenya kufuatia mgogoro unaoendelea baina ya Shirikisho la Soka Kenya (FKF) na Kampuni inayosimamia Ligi Kuu (KPL).
    KPL chini ya Mwenyekiti wake, Ambrose Rachier ambaye pia ni Mwenyekiti wa Gor Mahia, imekwishaandaa Ligi Kuu, lakini FKF chini ya Rais wake, Sam Nyamweya imeikana Ligi hiyo- huku nayo ikiandaa ligi yake.
    FKF wamesema Ligi Kuu yao itaanza wikiendi hii, wakati KPL wamesema Ligi Kuu halisi ya Kenya itaanza Februari 21, mwaka huu.
    Katika mchezo wa leo, kikosi cha Gor Mahia kilikuwa;Boniface Olouch, Godfrey Walusimbi, Abouba Sibomana, Mussa Mohammed, Khalid Aucho, Victor Abondo/Timoth Otieno, Ernest Wendo, Ronald Otieno/Innocent Wafula na Glay Dirkir, Abdul Nzigiyimana na Michael Olunga.
    Sofapaka; David Okello, Felly Mulumba, Collins Shivachi, Ekaliana Ndolo, Willis Ouma, Abdul Yorou, Maurice Odipo, Kevin Omondi/Shafiq Batambuze, Danson Kago/Elly Asieche, Enock Agwanda na Fiston Abdul Razack.   
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: GOR MAHIA WAITWANGA SOFAPAKA NA KUBEBA ‘SUPER CUP’ YA KENYA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top