Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
WACHEZAJI wawili wa waliokuwamo kwenye kikosi cha Uganda, The Cranes kilichocheza mechi za kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika mwakani, beki Juuko Murushid na mshambuliaji Simon Sserunkuma wamejiunga na Simba SC kwa majaribio.
Juuko aliwasili jana usiku Dar es Salaam, wakati Ivan ametua mchana wa leo pamoja na Nahodha wa Wekundu hao wa Msimbazi, Joseph Owino.
Kutua kwa wachezaji hao, kunapunguza nafasi ya Mkenya, David Owino ‘Calabar’ kusajiliwa kwenye kikosi cha Simba SC.
Huyo ni kwa sababu Sserunkuma wa Express ya Uganda na Juuko aliyewahi kucheza soka ya kulipwa nchi za Asia, kwa sasa ni wachezaji huru, wakati kwa Owino Simba SC italazimika kuilipa klabu yake, Gor Majia.
BIN ZUBEIRY inafahamu kwamba Owino amekwishatumiwa tiketi na Simba SC aje Tanzania, lakini amekuwa akikwamishwa na tatizo la usafiri.
Aidha, pamoja na Simba SC kukubaliana na Mtibwa Sugar kuuziana beki Hassan Ramadhani Kessy, lakini mchezaji huyo ametaka dau kubwa ambalo Wekundu hao wa Msimbazi ‘wanajifikiria’ kutoa.
WACHEZAJI wawili wa waliokuwamo kwenye kikosi cha Uganda, The Cranes kilichocheza mechi za kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika mwakani, beki Juuko Murushid na mshambuliaji Simon Sserunkuma wamejiunga na Simba SC kwa majaribio.
Juuko aliwasili jana usiku Dar es Salaam, wakati Ivan ametua mchana wa leo pamoja na Nahodha wa Wekundu hao wa Msimbazi, Joseph Owino.
Kutua kwa wachezaji hao, kunapunguza nafasi ya Mkenya, David Owino ‘Calabar’ kusajiliwa kwenye kikosi cha Simba SC.
Huyo ni kwa sababu Sserunkuma wa Express ya Uganda na Juuko aliyewahi kucheza soka ya kulipwa nchi za Asia, kwa sasa ni wachezaji huru, wakati kwa Owino Simba SC italazimika kuilipa klabu yake, Gor Majia.
Juuko Murushid tayari yuko kambini Zanzibar |
BIN ZUBEIRY inafahamu kwamba Owino amekwishatumiwa tiketi na Simba SC aje Tanzania, lakini amekuwa akikwamishwa na tatizo la usafiri.
Aidha, pamoja na Simba SC kukubaliana na Mtibwa Sugar kuuziana beki Hassan Ramadhani Kessy, lakini mchezaji huyo ametaka dau kubwa ambalo Wekundu hao wa Msimbazi ‘wanajifikiria’ kutoa.
0 comments:
Post a Comment