MABINGWA wa Afrika, Nigeria leo wametema rasmi taji baada ya kushindwa kufuzu kwenye Fainali zijazo za Mataifa ya Afrika kufuatia kulazimishwa sare ya 2-2 nyumbani na Afrika Kusini katika mchezo wa Kundi A.
Bafana Bafana imeifanyia 'roho mbaya' tu Nigeria kwani ilikuwa imekwishafuzu na katika mchezo wa leo, iliongoza muda mrefu kwa mabao 2-0 kabla ya wenyeji kusawazisha dakika za mwishoni.
Nigeria sasa haitakwenda Equatorial Guinea Januari mwakani kutetea taji lao, baada ya Kongo kuilaza 1-0 Sudan mjini Kharotum na kuungana na Bafana kwenda AFCON, huku Super Eagles ikimaliza katika nafasi ya tatu.
Bafana Bafana imeifanyia 'roho mbaya' tu Nigeria kwani ilikuwa imekwishafuzu na katika mchezo wa leo, iliongoza muda mrefu kwa mabao 2-0 kabla ya wenyeji kusawazisha dakika za mwishoni.
Nigeria sasa haitakwenda Equatorial Guinea Januari mwakani kutetea taji lao, baada ya Kongo kuilaza 1-0 Sudan mjini Kharotum na kuungana na Bafana kwenda AFCON, huku Super Eagles ikimaliza katika nafasi ya tatu.
Mabingwa wa Afrika, Nigeria wametemeshwa taji mapema leo |
0 comments:
Post a Comment