• HABARI MPYA

        Thursday, November 13, 2014

        NEYMAR AFUNGA MARA MBILI BRAZIL IKIICHAPA 4-0 UTURUKI SUKRU SARACOGLU

        NYOTA wa Barcelona, Neymar amefunga mabao mawili katika ushindi wa 4-0 wa timu yake ya taifa, Brazil dhidi ya Uturuki usiku wa kuamkia leo Uwanja wa Sukru Saracoglu.  
        Neymar aliwafungia bao la kwanza mabingwa hao mara tano wa Kombe la Dunia dakika ya 20, kabla ya beki wa Uturuki, Semih Kaya kujifunga kuipatia Brazil bao la pili dakika ya 24.
        Willian akawafungia Brazil bao la tatu dakika ya 44, kabla ya Nahodha Neymar kuhitimisha ‘pati la mabao’ kwa kuifunga bao la nne timu ya Carlos Dunga dakika ya 60.
        Kikosi cha Uturuki kilikuwa; Demirel, Kaya, Koybasi, Irtegun, Tufan, Kisa, Altintop, Turan, Topal, Bulut na Erdinc. 
        Brazil: Diego Alves, Danilo, Miranda, Luiz, Luis, Fernandinho, Oscar, Gustavo, Willian, Luiz Adriano na Neymar. 
        Brazil captain Neymar scored twice in their 4-0 international friendly victory away to Turkey on Wednesday
        Nahodha wa Brazil, Neymar akisherehekea baada ya kufunga mabao mawili katika ushindi wa 4-0 jana dhidi ya wenyeji Uturuki
        Neymar (right) completed the scoreline on the hour mark after he rounded Demirel before finishing
        Neymar (kulia) akijiandaa kumfunga kipa Demirel 

        PICHA ZAIDI NENDA: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-2832023/Turkey-0-4-Brazil-Neymar-scores-twice-Semih-Kaya-goal-Willian-strike-wrap-easy-friendly-win-visitors.html#ixzz3IuZu5r4B 
        • Blogger Comments
        • Facebook Comments

        0 comments:

        Item Reviewed: NEYMAR AFUNGA MARA MBILI BRAZIL IKIICHAPA 4-0 UTURUKI SUKRU SARACOGLU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry