BONDIA Manny Pacquiao has laid the gaamesema kwamba Floyd Mayweather, nyota wa ndondi Mmarekani ndiye anayegoopa pambano baina yao.
Pambano baina ya Mayweather na Pacquiao tayari limepewa had hi ya 'Pambano la Mabilioni ya Dola', lakini bingwa huyo wa dunia amesema hatakasirika iwapo halitaokea.
Akizungumza na Daily Telegraph, Pacquiao amesema: "SitapagawaI iwapo pambano na Floyd halitatokea,".
Manny Pacquiao (kushoto) amesema Floyd Mayweather amekuwa akikataa ku[igana naye
"Nafikiri niko tayari kupigana naye wakayti wowote, mahali popote- ni yeye ndiye anayekataa. Nimeweka hii wazi kwamba nataka kupigana naye- ni juu yake sasa. Ni dhahiri anaogopa kupigana na mimi. Wakati wote anatoa sababu. Kubali pambano na acha kuchonga,". amesema.
Pacquiao, ambaye atapigana na Mmarekani mwingine, Chris Algieri mjini Macau Jumamosi, pia amemkandia Mayweather na tania yake ya kusambaza fedha zake na kupiga picha kuweka kwenye mitandao ya kijamii.
Pacquiao amesema: "Napingana naye, kwa sababu yote anayofikiria na kufanya yanaleta mitazamo tofauti kwenye maisha ya dunia yetu. Anaonekana kusahau asili yake,".
Mayweather mara ya mwisho alimpiga Marcos Maidana mjini Las Vegas mapema mwaka huu
0 comments:
Post a Comment