HABARI njema kwa Manchester United ni kwamba, kipa wao David De Gea anaweza kurejea kazini kwenye kikosi cha kocha Louis van Gaal Jumamosi watakapoifuata Arsenal.
De Gea aliuamia kidole chake kidogo akiwa na timu yake ya taifa, Hispania wiki iliyopita na pamoja na hofu ya awali kwamba kingemuweka nje kwa muda mrefu, lakini sasa inabainika mlinda mlango huyo anaweza kuwa kazini Uwanja wa Emirates Jumamosi.
Chanzo kutoka ndani ya timu ya taifa ya Hispania kimeithibitishia Daily Mail jana jioni kwamba De Gea ana asilimia 80 ya kuwa fiti na kuanza kwenye kikosi cha kwanza cha United kitakachomenyana na Arsenal katika mchezo wa Ligi Kuu ya England mwishoni mwa wiki.
De Gea atachunguzwa na timu ya matabibu wa United na kocha wa makipa, Frans Hoek kama atakuwa fiti kudaka dhidi ya Arsenal Jumamosi
0 comments:
Post a Comment