// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); BABU HOPKINS ASEMA ANATAKA PAMBANO MOJA ZAIDI, TENA NA BONDIA MKALI - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE BABU HOPKINS ASEMA ANATAKA PAMBANO MOJA ZAIDI, TENA NA BONDIA MKALI - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
    Wednesday, November 12, 2014

    BABU HOPKINS ASEMA ANATAKA PAMBANO MOJA ZAIDI, TENA NA BONDIA MKALI

    BONDIA mkongwe Bernard Hopkins atarejea ulingoni licha ya kipigo cha mwishoni mwa wiki kutoka kwa Mrusi, Sergey Kovalev, amesema babe huyo mwenye umri wa miaka 49 jana.
    Hopkins, ambaye alishindwa kushinda hata raundi moja katika pointi za majaji wote matatu kwenye pambano hilo la uzito wa Light-Heavy la kuunganisha mataji, amezima tetesi za kustaafu kwake kwa kusema atapigana 'mara moja zaidi.'
    "Nani nitapigana naye? Sijui,"amesema Hopkins katika mahojiano ya simu kutoka nyumbani kwake, Delaware. "Lakini atakuwa mtu fulani ambaye ni mkali, na ninataka kupigana na mkali,".
    Former world champion Bernard Hopkins insists he will fight 'one more time' before retirement 
    Bingwa wa zamani wa dunia, Bernard Hopkins amesema atapigana 'mara moja zaidi' kabla ya kustaafu
    Sergey Kovalev knocks down Hopkins in the first round on his way to a comprehensive victory
    Sergey Kovalev akimpeleka chini Hopkins katika raundi ya kwanza, ingawa alifanikiwa kumaliza raundi 12
    Hopkins falls to the canvas in the opening stages after being caught by a right hand to the top of the head
    Hopkins akiwa ameanguka chini baada ya konde la mpinzani wake

    Hopkins, aliyefanikiwa kutetea vizuri kwa rekodi ubingwa wa uzito wa Middle mara 20 kuanzia mwaka 1995 hadi 2005 na hajawahi kuangushwa chini kabla, lakini aliangushwa kwa mara ya kwanza Jumamosi katika raundi ya kwanza na Kovalev.
    Pamoja na hayo alisimama na kuendelea na pambano hadi kupoteza kwa pointi dhidi ya kijana huyo aliyemzidi umri wa miaka 18.
    Na huwezi kuamini, bondia huyo anayejulikana kwa nina la utani kama The Executioner alirudi mazodzi tena gym Jumatatu, yaani wastani wa siku moja baada ya pambano lake.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BABU HOPKINS ASEMA ANATAKA PAMBANO MOJA ZAIDI, TENA NA BONDIA MKALI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry