// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); AZAM YABANWA NA POLISI, SARE 1-1 CHAMAZI - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE AZAM YABANWA NA POLISI, SARE 1-1 CHAMAZI - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

        Friday, July 25, 2014

        AZAM YABANWA NA POLISI, SARE 1-1 CHAMAZI

        Na Prince Akbar, DAR ES SALAAM
        AZAM FC imelazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Polisi Morogoro iliyopanda Ligi Kuu msimu huu katika mchezo wa kirafiki asubuhi ya leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
        Mshambuliaji Danny Mrwanda aliyekuwa anacheza Vietnam, alianza kuifungia Polisi Morogoro kabla ya mshambuliaji kutoka Haiti, Leonel Saint-Preux kuisawazishia Azam, mabao yote yakipatikana kipindi cha kwanza.
        Kipre Balou akiwakimbiza viungo wa Polisi, huku kaka yake Kipre Tchetche akiwa tayari kumsaidia
        Kipre Balou akifanya vitu adimu pembeni ya wachezaji wa Moro
        David Mwantika akikosa bao la wazi baada ya kupanda kusaidia mashambulizi
        Kipre Tchetche akitafuta mbinu za kumtoka beki wa Polisi
        Didier Kavumbangu akimiliki mpira mbele ya beki wa Polisi
        Gaudence Mwaikimba akimiliki mpira mbele ya beki wa Polisi

        Polisi inayofundishwa na kiungo wa zamani wa kimataifa wa Tanzania, Mohamed ‘Adolph’ Rishard ilicheza soka ya kuvutia dhidi ya Azam FC, ambao ni mabingwa wa Ligi Kuu. 
        Washambuliaji wote wa kigeni wa Azam FC, Ismaila Diara kutoka Mali, Didier Kavumbangu kutoka Burundi, Leonel Saint-Ptreux kutoka Haiti walicheza pamoja na beki Mghana Ben Achaw na viungo Serge Lofo kutoka DRC na Joseph Peterson wa Haiti.
        Huo unakuwa mchezo wa kwanza katika mechi za kujiandaa na msimu Azam inashindwa kuondoka na ushindi, baada ya awali kuzifunga 1-0 Ruvu Shooting, 2-1 Friends Rangers, 3-2 kombaini ya Jeshi, 1-0 Polisi Morogoro na 2-1 JKT Ruvu.
        Kikosi cha Azam kinakwenda mapumziko ya sikukuu ya Eid El Fitri na kinatarajiwa kurudi mazoezini kuanzia Jumatano wiki ijayo.

        • Blogger Comments
        • Facebook Comments

        0 comments:

        Item Reviewed: AZAM YABANWA NA POLISI, SARE 1-1 CHAMAZI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry