ITALIA NJE KOMBE LA DUNIA, SUAREZ ANG'ATA MTU TENA, ENGLAND YAAMBULIA POINTI BRAZIL
ITALIA imeaga Kombe la Dunia nchini Brazil baada ya kufungwa 1-0 na Uruguay, bao pekee la Diego Godin katika mchezo ambao mshambuliaji Luis Suarez alimng’ata Giorgio Chiellini. Godin alifunga bao hilo dakika ya 81 na kipa Buffon wa Italia alilazimika kuingia uwanjani dakika ya mwisho kusaidia nguvu ya kusaka bao, Azzuri ikihtaji sare tu kusonga mbele. Italia ilimpoteza mchezaji wake Marchisio aliyetolewa kwa kadi nyekundu baada ya kumchezea rafu Arevalo Rios dakika ya 60.
Mkongwe wa Italia, Andrea Pirlo (kushoto) akibadilishana jezi na Edisnon Cavani wa Uruguay baada ya mechi
Suarez baada ya kumng'ata Chiellini
Refa hakumpa adhabu Suarez
Chiellini akilalamika kung'atwa na Suarez begani
Costa Rica imemaliza kileleni mwa Kundi D baada ya sare ya 0-0 na England leo ikifikisha pointi saba, Uruguay pointi sita na Italia pointi tatu, wakati England imeondoka na pointi moja. Kikosi cha Italia kilikuwa; Buffon, Barzagli, Bonucci, Chiellini, Marchisio, De Sciglio, Verratti/Motta dk75, Pirlo, Darmian, Balotelli/Parolo dk46 na Immobile/Cassano dk71. Uruguay: Muslera, Caceres, Gimenez, Godin, A.Pereira/Stuani dk63, Gonzalez, Arevalo Rios, Rodriguez/Ramirez dk78, Lodeiro/M Pereira dk46, Cavani na Suarez.
Azu third as Simbine wins 100m in Xiamen
-
Great Britain's Jeremiah Azu finishes third in the men's 100m behind South
Africa's Akani Simbine and Kenya's Ferdinand Omanyala at Diamond League
Xiamen.
Reports: Jack Wilshere set for Arsenal return
-
Former Arsenal midfielder Jack Wilshere has held talks with the north
London side on one of its vacant academy coaching roles. Under 23 manager
Per Mertes...
YANGA ‘KUPAA’ JUMANNE KUIFUATA MWADUI FC
-
MARA baada ya mchezo wa kirafiki dhidi ya Namungo Fc kwenye uwanja wa
Majaliwa, Lindi, siku ya jumapili, Kikosi cha Young Africans Sports Club,
kitareje...
0 comments:
Post a Comment