Watafunga wengine leo, si wewe; Beki wa Simba SC, Hassan Hatibu akimkwatua mshambuliaji wa Azam FC, John Bocco 'Adebayor' anayekwenda chini katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Azam FC ilishinda 2-1.
Winga wa Azam FC, Joseph Kimwaga alikaribia kufunga leo kama anavyoonekana hapa akikosa bao la wazi licha ya kufanikiwa kuwatoka mabeki na kumpiga chenga kipa Abbel Dhaira
Hassan Hatibu akipambana na John Bocco
John Bocco pia alikosa bao la wazi kufuatia krosi nzuri ya Joseph Kimwaga ambayo alishindwa kuunganisha ikapitiliza
Issa Rashid 'Baba Ubaya' alimkaba sana Kipre Tchetche pamoja na kufungwa mabao yote ya Azam FC leo
Mfungaji wa bao la Simba SC, Ramadhani Singano 'Messi' akienda chini baada ya kupamiwa na Humphrey Mieno wa Azam FC
Betram Mombeki wa Simba SC akipambana na Erasto Nyoni wa Azam
Zahor Pazi wa Simba akipambana na Humphrey Mieno wa Azam
KIpre Tchetche akimfunga tela William Lucian 'Gallas'
Mzee bomoa benki, usajii hapa huna timu; Katibu Mkuu wa zamani wa Simba SC, Kassim Dewji akizungumza na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe kulia
Namna watu wanvyofuatilia mchezo kwa umakini, na hii mara nyingi hutokea timu yao inapokuwa imefungwa
Farid Mussa naye alikosa bao la wazi baada ya kuingia akitokea benchi
Kipre Tchetche akimtoka Baba Ubaya
Salum Abubakar 'Sure Boy' alimvisha kanzu saizi yake Amri Kiemba
Kipa wa Simba SC akidaka mpira juu ya kichwa cha mshambuliaji wa Azam FC, John Bocco huku mabeki wake wakiwa tayari kumsaidia
Mehmet Ali on West Brom defeat
-
Mehmet Ali looked ahead to the Premier League 2 Playoffs after a 4-3 defeat
to West Brom in our final regular season game.
Aspiring football agents to enroll for FIFA exams
-
The 5th FIFA Football Agent Exam is set to take place on 18th June 2025,
and registration is now open for aspiring football agents. The exam, which
will ...
Reports: Jack Wilshere set for Arsenal return
-
Former Arsenal midfielder Jack Wilshere has held talks with the north
London side on one of its vacant academy coaching roles. Under 23 manager
Per Mertes...
YANGA ‘KUPAA’ JUMANNE KUIFUATA MWADUI FC
-
MARA baada ya mchezo wa kirafiki dhidi ya Namungo Fc kwenye uwanja wa
Majaliwa, Lindi, siku ya jumapili, Kikosi cha Young Africans Sports Club,
kitareje...
0 comments:
Post a Comment