Gwiji hai: Shujaa wa Argentina, Diego Maradona alikuwepo kwenye kipindi cha maswali na majibu mjini Milan Jumatano
GWIJI wa soka duniani, Diego Maradona amesema kwamba Mario Balotelli ni mwanasoka nambari nne kwa ubora hivi sasa duniani baada ya Messi, Ronaldo na Neymar.
Katika kipindi cha maswali na majibu mjini Milan, gwiji huyo wa Argentina alielezea mapenzi yake kwa nyota huo wa zamani wa Manchester City na kwamba walianza kufahamiana vyema na mshambuliaji huyo wa Italia alipomtumia picha anavuta cigar ya Cuba.
Namba 10 huyo wa zamani, mmoja wa wanasoka bora kabisa kuwahi kutokea duniani alisema: "Mawasiliano yangu ya kwanza na Mario ni pale aliponitumia picha yake anavuta Cuban. Naipenda! Nilicheza,".
Maradona pia anataka kukutana na Balotelli ili ampe ushauri nasaha mshambuliaji huyo wa AC Milan.
"[Watu lazima] wamuache na amani. Ningependa kuzungumza na Mario peke yetu, katika chumba chetu, na kumfafanulia uzoefu mbaya wote niliopitia.'
Watu wa vituko: Maradona anapenda kuzungumza na Balotelli na kumpa uzoefu wa maisha mabovu aliyopitia katika mchezo huo
Namba moja: Maradona amesema Muargentina mwenzake Lionel Messi mwanasoka bora namba moja na Balotelli ni wa nne
Pamoja na hayo, licha ya kuwa shabiki mkubwa wa Balotelli, Maradona anampa nafasi ya nne mshambuiaji huyo wa Milan katika orodha yake ya wachezaji bora duniani, akimuweka nyuma ya Lionel Messi, Cristiano Ronaldo na Neymar.
Wakati huo huo, nyota huyo wa zamani wa Napoli amesema kwamba anapenda kurudi katika klabu hiyo kama kocha mara kocha wa sasa, Rafa Benitez atakapoondoka.
Akiwa ameshinda mataji mawili ya Serie A na timu hiyo miaka ya 1987 na 1990, Nyota huyo wa Amerika Kusini amesema: "Wakati (Rafa) Benitez atakapoondoka ningependa kuikochi Napoli,".
Alama ya Napoli: Timu hiyo ya Italia ilishinda mataji ya Serie A mwaka 1987 na 1990 ikiongozwa na Maradona
Kitimoto: Kocha wa zamani wa Liverpool na Chelsea, Rafa Benitez (kulia) kwa sasa anaifundisha Napoli ya Italia aliyojiunga nayo msimu huu
Pamoja na hayo, mtu mzima huyo mwenye umri wa miaka 52 si rahisi sana kwake kupata nafasi hiyo: "Kuna mabadiliko ya makocha yanafanyika kila sehemu kutoka Hispania hadi Italy hadi England hadi Urusi, lakini watu fulani wananiogopa mimi. Ndiyo maana sikochi,."
Maradona aliifundisha Argentina hadi kuifikisha Robo Fainali ya Kombe la Dunia mwaka 2010 na kisha akaenda Dubai kufundisha klabu ya Al Wasl kwa msimu mmoja.
Anatoa pointi: Akiwa ameifundisha Argentina katika Fainali za Kombe la Dunia 2010 (chini), Maradona amesema hafundishi kwa sasa kwa sababu watu fulani wanamuogopa
0 comments:
Post a Comment