• HABARI MPYA

        Wednesday, September 25, 2013

        NEYMAR, MESSI WAFUNGA WOTE BARCA IKIUA 4-1 LA LIGA

        IMEWEKWA SEPTEMBA 25, 2013 SAA 12:31 ASUBUHI
        WACHEZAJI nyota duniani, Neymar na Lionel Messi wote walifunga mabao jana kwa mara ya kwanza wakati Barcelona inaendeleza wimbi lake la ushindi La Liga kufuatia ushindi wa 4-1 dhidi ya Real Sociedad Uwanja wa Nou Camp.
        Barcelona imeendeleza rekodi nzuri katika harakati za kutetea taji, huku Neymar akifunga bao lake la kwanza La Liga na Messi akifunga bao lake la saba msimu huu.
        Neymar alifungua karamu ya mabao ya Barca dakika ya tano, kabla ya Messi kufunga la pili dakika tatu baadaye, Busquets la tatu dakika ya 23 na Bartra kuhitimisha dakika ya 77.
        Bao pekee la kufutia machozi la wageni lilifungwa na De la Bella dakika ya 64.
        Kikosi cha Barcelona jana kilikuwa: Valdes; Alves, Pique, Mascherano, Adriano; Busquets, Xavi, Iniesta; Sanchez, Messi na Neymar.
        Real SociedadBravo; Estrada, Cadamuro, Martinez, De la Bella; Bergara, Ros, Prieto, Sangalli; Seferovic, Griezmann.
        Lionel Messi
        Wawili, mawili: Lionel Messi akishangilia bao lake alilotengenezewa nafasi ya kufunga na Mbrazil, Neymar 
        Neymar
        La kwanza kati ya mengi: Neymar akipiga ngumi hewani kushangilia bao lake la kwanzkufunga La Liga
        Neymar
        Kijana kutoka Brazil: Neymar akipongezwa na wachezaji wenzake 
        BARCELONA
        Neymar
        Hisi upendo: Neymar na Messi wakionyesha watoto wao kabla ya mechi na kulia wakipongezana baada ya mechi
        Sergio Busquets
        Mtu mrefu: Sergio Busquets (katikat) akiwapa tano wenzake baada ya kufunga
         Lionel Messi
        Mashine: Lionel Messi akijaribu kupasua ukuta wa Sociedad 
        Marc Bartra
        Bao la mwisho: Beki wa Barca, Marc Bartra (wa pili kushoto) alihitimisha karamu ya mabao ya Barca kwa bao la nne
        Barcelona
        Mchuano: Sergio Busquets (kushoto) akigombea mpira na mshambuliaji wa Real Sociedad, Imanol Agirretxe
        Barcelona
        Kazi kazi: Andres Iniesta (kulia) akipambana na Inigo Martinez Berridi
        Barcelona
        Gerard Pique (kushoto) akimtoka kiungo wa Sociedad, Markel Bergara Larranaga 
        Alexis Sanchez
        Alexis Sanchez wa Barca akigombea mpira na Alberto de la Bella
        • Blogger Comments
        • Facebook Comments
        Item Reviewed: NEYMAR, MESSI WAFUNGA WOTE BARCA IKIUA 4-1 LA LIGA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry