• HABARI MPYA

        Saturday, September 21, 2013

        CHELSEA YAUA 2-0...OBI MIKEL AFUNGA BAO LA KWANZA LIGI KUU ENGLAND, MOURINHO AENDELEZA REKODI YA KUTOFUNGWA NDANI YA MECHI 63 DARAJANI

        IMEWEKWA SEPTEMBA 21, 2013 SAA 3:59 USIKU
        KIUNGO John Obi Mikel amefunga bao lake la kwanza katika Ligi Kuu ya England na kuiwezesha Chelsea kuibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya Fulham Uwanja wa Stamford Bridge, huo ukiwa ushindi wao wa kwanza mwezi huu.
        Mabao ya Oscar na Mikel kipindi cha pili yamemaliza ukame wa ushindi ndani ya mechi nne na kuendeleza rekodi ya Jose Mourinho kutofungwa nyumbani katika Ligi Kuu ndani ya mechi 63 na ushndi wa kwanza tangu wafungwe na Aston Villa.
        Ushindi huo wa 2-0 unamaanisha Fulham inatimiza miaka 34 bila kushinda Stamford Bridge, Chelsea ikizinduka baada ya vipigo vya Everton na Basle.
        Kikosi cha Chelsea kilikuwa: Cech, Ivanovic, Cahill, Terry, Cole, Ramires, Mikel, Schurrle/Lampard dk79, Oscar, Hazard/De Bruyne dk85, Eto’o/Torres dk64.
        Fulham: Stockdale, Riether, Amorebieta, Hangeland, Richardson, Duff/Taarabt dk64, Parker, Sidwell, Kacaniklic/Tue Na Bangna dk72, Kasami/Rodallega dk85 na Bent.
        Back to winning ways: Oscar celebrates his goal - Chelsea's first in more than four hours of Premier League football
        Ushindi umerudi: Oscar akishangilia bao lake na wenzake
        On target: Oscar breaks the deadlock at Stamford Bridge
        Oscar amefunga bao la kwanza leo Stamford Bridge
        A rarity: John Obi Mikel stretches to score his first goal for 258 matches
        Bao tamu sana: John Obi Mikel akifunga bao lake la kwanza Ligi Kuu England baada ya mechi 258
        Ecstatic: The midfielder was delighted with his goal
        Raha sana: Obi akishangilia bao lake
        Back to winning ways: Jose Mourinho celebrated his first win in a month
        Raha zimerejea Darajani: Jose Mourinho akishangilia ushindi wake wa kwanza mwezi huu
        Slightly better: Roman Abramovich was in the stands again to watch the victory
        Mwenye timu tabasamu latosha: Roman Abramovich akiwa jukwaani kuangalia ushindi wa timu yake
        Golden: Darren Bent missed a brilliant chance when the game was still 0-0
        Amekosa: Darren Bent alipoteza nafasi nzuri ya kufunga wakati timu hizo hazijafungana
        In pain: Scott Parker is felled by Gary Cahill
        Maumivu: Scott Parker akichezewa rafu na Gary Cahill
        Flattened: Steve Sidwell leaves Eden Hazard on the floor after a challenge
        Hdi chini: Steve Sidwell akimuacha chini Eden Hazard baada ya kugombea naye mpira
        Drawing a blank: Samuel Eto'o again failed to find the mark for his new club
        Mabao wapi?: Samuel Eto'o kwa mara nyingine ameshindwa kuifungia timu yake mpya
        Up in the air: John Terry directs the ball towards goal from a corner
        John Terry akiwania mpira wa juu
        Under pressure: Branislav Ivanovic is closed down by Pajtim Kasami
        Branislav Ivanovic akipambana na Pajtim Kasami
        Battle: Ramires, attempts to tackle Alexander Kacaniklic
        Ramires, akipambana na Alexander Kacaniklic
        • Blogger Comments
        • Facebook Comments
        Item Reviewed: CHELSEA YAUA 2-0...OBI MIKEL AFUNGA BAO LA KWANZA LIGI KUU ENGLAND, MOURINHO AENDELEZA REKODI YA KUTOFUNGWA NDANI YA MECHI 63 DARAJANI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry