• HABARI MPYA

        Thursday, August 01, 2013

        BAYERN MUNICH YAILAZA SAO PAOLO 2-0 NA KUTINGA FAINALI KOMBE LA AUDI, SASA KUUMANA NA MAN CITY

        IMEWEKWA AGOSTI 1, 2013 SAA 7: 00 USIKU
        KLABU ya Bayern Munich imeifunga Sao Paulo mabao 2-0 katika michuano yao ya Kombe la Audi Cup na kuungana na Manchester City katika fainali itakayopigwa Uwanja wa Allianz Arena.
        Sasa kocha Pep Guardiola anajiandaa kukabiliana na timu yenye safu kali ya ushambuliaji, City ambayo mapema iliikung'uta AC Milan 5-3 katika mchezo wa kwanza.
        Mabao yote Bayern yalipatikana kipindi cha pili, wafungaji Mario Mandzukic na kinda Mitchell Weiser ingawa na wageni walipata nafasi ya kufunga baadaye, lakini kipa Rogerio Ceni akakosa penalti. Thiago Alcantara aliachwa nje na kocha Guardiola.
        Goalscorers: Mandzukic (above) and Mitchell Weiser (below) are congratulated after their goals
        Wafungaji wa mabao: Mario Mandzukic (juu) na Mitchell Weiser (chini) wakipongezana
        Goalscorers: Mandzukic (above) and Mitchell Weiser (below) are congratulated after their goals
        Katika mchezo ambao walifungwa mabao 4-2 na Dortmund kuwania Super Cup ya Ujerumani, Thiago, ambaye alikuwa anawaniwa na Manchester United majira haya ya joto, alipigwa kibao na Guardiola.
        • Blogger Comments
        • Facebook Comments
        Item Reviewed: BAYERN MUNICH YAILAZA SAO PAOLO 2-0 NA KUTINGA FAINALI KOMBE LA AUDI, SASA KUUMANA NA MAN CITY Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry