// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); YANGA NA AZAM KUWANIA NGAO AGOSTI 17 TAIFA, LIGI KUU KUANZA AGOSTI 24 - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE YANGA NA AZAM KUWANIA NGAO AGOSTI 17 TAIFA, LIGI KUU KUANZA AGOSTI 24 - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

        Monday, July 22, 2013

        YANGA NA AZAM KUWANIA NGAO AGOSTI 17 TAIFA, LIGI KUU KUANZA AGOSTI 24

        Na Boniface Wambura, IMEWEKWA JULAI 22, 2013 SAA 6:10 MCHANA
        LIGI Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu wa 2013/2014 inaanza kutimua vumbi Agosti 24 mwaka huu kwa timu zote 14 kuwa viwanjani katika miji saba tofauti.
        Hata hivyo, kabla ya ligi hiyo kuanza kutakuwa na mechi ya kufungua msimu (Ngao ya Jamii- Community Shield) kati ya bingwa mtetezi Yanga na Makamu bingwa Azam itakayochezwa Agosti 17 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
        Inavyokuwaga; Yanga na Azam katika mechi ya Ligi Kuu msimu uliopita

        Mechi za VPL za Agosti 14 mwaka huu zitakuwa kati ya Yanga na Ashanti United (Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam), Mtibwa Sugar na Azam (Uwanja wa Manungu, Morogoro), na JKT Oljoro na Coastal Union (Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid, Arusha).
        Nyingine ni Mgambo Shooting na JKT Ruvu (Uwanja wa Mkwakwani, Tanga), Rhino Rangers na Simba (Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora), Mbeya City na Kagera Sugar (Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine, Mbeya), na Ruvu Shooting na Tanzania Prisons (Uwanja wa Mabatini, Mlandizi, Pwani).
        Mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo utamalizika Novemba 3 mwaka huu wakati wa pili utamalizika Aprili 27 mwakani. (Ratiba ya mzunguko wa kwanza na wa pili imeambatanishwa- kulia angalia).

        • Blogger Comments
        • Facebook Comments
        Item Reviewed: YANGA NA AZAM KUWANIA NGAO AGOSTI 17 TAIFA, LIGI KUU KUANZA AGOSTI 24 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry